Chuki na lawama ni mambo ambayo yanakuja kwa kasi sana katika maisha ya jamii zetu. Mbaya zaidi, katika mahali pa kazi, hayo yameanza kuwa ndio maisha ya wengi. Kwenye sehemu ya kazi, chuki huja kuhusiana na utendaji wa kazi wa mtu. Kuna ambaye anachukiwa tu kwa sababu ya utendaji wake wa kazi na umakini katika kuitenda kazi aliyokabidhiwa na mkuu wake wa kazi.
Tag Archives: Tanzania
Hakuna Marefu Yasiyokuwa Na Ncha
Maisha ni mzunguko, na sisi binadamu tunapoishi hapa duniani, tunakutana na mambo mengi sana yakiwemo mazuri na mengine mabaya, ya kusikitisha na hata yanayofurahisha.
Ukubwa Ni Jaa
Jaa ni jalala, mahali ambapo watu hutupa taka taka zao. Kwa hiyo mtu mkubwa ni kama jaa, kila mwenye takataka zake, (matusi, lawama, n.k) humtupia yeye.
Adui Hatoki Mbali
Usemi huu unatufundisha jinsi tunavyopaswa kuishi na jamii na marafiki wanaotuzunguka. Ni vizuri kuwa karibu na hao watu kwa sababu hata maandiko yamesema binadamu tupendane na tusaidiane. Tunapaswa kujua kuwa hayo yote tunatakiwa tuyafanye kwa kiasi na kwa makini sana. Kumbuka, wema wako unaweza kukupeleka kwenye kilio. Sio kilio cha kufiwa, bali tunaongelea kilio kitokanacho na matatizo utakayoyapata baada ya hapo.
Usitunze Huzuni Moyoni
Huzuni ni hali ya masikitiko yenye masononeko inayomfanya mtu akose furaha, amani na matumaini kwa kiwango kikubwa na kwa muda mrefu. Hali hiyo humfanya mtu atawaliwe na mawazo mengi sana, ikiwa pamoja na msongo wa mawazo na sonona. Inapokithiri bila kupata huduma sahihi huweza kusababishahta kifo.
Usitoe Maamuzi Wakati Una Furaha Sana
Tuko katika ulimwengu wenye vurugu na fujo zisizohesabika. Kila mtu anacho akijuacho ambacho anaona mwingine hakijui na wala hakiwezi. Ni fikira ambazo wanadamu tunatembea nazo. Furaha na huzuni ni sehemu ya maisha yetu.
Mtu Hufurahia Shida Zako, Sio Furaha Yako
Matatizo yameumbwa na kila mtu huyapata. Hakuna mtu ambaye hajawahi kupitia matatizo, na hayuko ambaye hatayapitia. Inategemea ni tatizo gani na wakati gani linakutokea.
Ishi Kadri Unavyojaliwa, Na Sio Kama Mwingine Anavyoishi
Watu wengi wana kawaida ya kupenda kujilinganisha na watu wengine. Watu kama hao hupenda kujiuliza, “kama yule yuko hivi, kwa nini na mimi nisiwe vile?”
Tujifunze Kusamehe
Alikuwepo mama mmoja ambaye alikuwa mwalimu wa shule ya msingi. Mama huyu alibahatika kupata mtoto wa Kike ambaye aliweza kumsomesha hadi Chuo Kikuu. Baada ya kuhitimu shahada yake, alimtafutia kazi nzuri.
Njia Ya Mkato Tamu, Lakini Ina Madhara
Mara nyingi kama mtu anataka afike haraka, anatafuta njia ya kukatisha, njia ya haraka. Njia hiyo inaweza kuwa nzuri pale tu utakapofanikiwa kufika kule uendako. Kuna wakati lakini njia ya mkato inaweza ikakupoteza na ukashindwa kufika uendako. Kuna baadhi ya binadamu, hupenda kutafuta mafanikio kwa kupitia njia ya udanganyifu, kama kutapeli wenzao.