Huo msemo niliujumuisha na usemi ambao tumezoea kuuzungumza. Msemo huo ni ule wa: ‘Sheria ni msumeno ambao unakata kote kote’. Nilishuhudia tukio hili nilipokuwa nasafiri toka Mwanza kuja Dar. Tulipofika Shinyanga tuliona abiria watatu wameingia kwenye basi tulilokuwemo. Mmoja wa abiria hao alikuwa amefungwa pingu.
Tag Archives: Tanzania
Tuchukue Tahadhari Stahiki, Dunia Inabadilika Kwa Kasi Mno
Ni ukweli usiopingika kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa sana kila kukicha, mithili ya mtu aliyegeuza miguu juu, kichwa chini. Dunia ya leo siyo kama ile ya zamani. Dunia ya sasa imekuwa na mambo mengi ya aibu, maovu ya kutisha na ya kusikitisha kiasi kwamba ubinadamu au utu umetoweka. Imefika mahali hatuna huruma tena, tumekuwa kama wanyama. Mambo mengi mabaya yanaibuka kila siku na hata usalama wa binadamu upo mashakani.
Maisha Mashenzi
Maisha ni zawadi ambayo Mungu ametupa wanadamu ili tuishi kwa mafanikio kadiri alivyotuahidi maana vyote chini ya jua ni vyetu kwa hiyo kila mtu awe na maisha mazuri na yenye baraka.
Penye Mafanikio Kuna Furaha
Shughuli yoyote ambayo mwanadamu anafanya ni kwa madhumuni ya kufanikiwa. Katika mafanikio hayo ndipo inazaliwa furaha. Daima ukiona mtu amefurahi sana, ukitafuta sababu utakuta kuwa kuna mahali amefanikiwa. Nyumba yeyote ambayo imejaa upendo, basi elewa kuwa pale pana mafanikio kwa njia moja au nyingine.
Heri Lawama Kuliko Fedheha
Lawama ni hali ya kulalamika kuhusu jambo ama tatizo fulani. Fedheha maana yake ni aibu. Mara nyingi watu hutumia muda wao mwingi kulalamikia ugumu wa maisha. Ukiwachunguza watu hao kwa undani utakuta ni wale ambao ni wavivu, wasiopenda kufanya kazi. Mara nyingi watu hao hushinda vijiweni na kuzungumza mambo ya umbea ambayo hayana tija kwao wala kwa jamii. Kati ya watu hawa huwa na dharau na kebehi, wasiotafuta fursa, wasiopenda kushirikiana na wenzao na wenye mtizamo hasi dhidi ya wenzao na wao wenyewe.
Mawazo Ya Watu Wenye Hekima Ni Kama Shamba
Hekima ni mojawapo ya vipaji ambavyo Muumba wetu hutoa kwa viumbe wake. Ieleweke kuwa, sio kila mtu anajaliwa kupata vipaji. Lakini endapo itatokea kuwa unataka kipaji basi unashauriwa kuwa ni vema ukaomba hekima.
Ziba Mwanya Usiruhusu Panya Kupita
Mwanya ni nafasi yoyote ambayo mtu au kitu kinaweza kupita au kupenyeza bila kizuizi. Unaweza kuwa mwanya mkubwa au mwanya mdogo, alimradi hauzuii kilichokusudiwa kupenyeza. Hii ina maana kuwa, jambo lolote linapoanza kuharibika, huanza kidogo kidogo au taratibu sana na wakati mwingine bila hata kutambua.
Mwongo Huwa Hasemi Yake
Mtu mwongo ni yule mtu ambaye anapenda kuongea mambo ya wenzake kwa ushabiki. Mara nyingi huwa anaongea katika mithili ya kumdhalilisha mtu. Watu wa aina hii huwa wana asili ya kuwa na marafiki wengi ambao huvutiwa na stori zake za uongo. Huo ni ubinadamu wa watu ambao hawajitambui. Mara nyingi, kinachofanyika hapo huwa ni unafiki mtupu.
Muda Haumsubiri Mvivu
Kila jambo lina wakati na majira yake. Hata tunapopanga mipango tunaweka na muda wa kutekeleza. Pamoja na hayo, inategemea na jinsi wewe mpangaji wa mipango kama unajali muda na wakati wa kuitekeleza. Usipozingatia utakuta muda umeondoka bila ya matokeo.
Tafuta Raha, Shida Zinakuja Zenyewe
Neno shida lina maana pana sana. Tunaweza kusema kuwa shida ni tatizo ambalo mtu anakuwa nalo. Mtu anaweza asijue namna ya kujinasua au namna ya kufanya ili aondokane nayo.