Tunajifunza umuhimu wa kuwa wavumilivu katika maisha yetu haijalishi tunapitia mazingira magumu kiasi gani. Maisha yana mapito mengi, yatupasa kutulia na kufanya maamuzi ya busara ili hatimaye tuweze kupata malipo ya uvumilivu wetu. Hata kama maisha tunayoishi hayatupatii yale tunayoyategemea, yatupasa kuendelea kuamini kuwa iko siku tutafanikiwa. Hakuna kisichowezekana chini ya jua.
Tag Archives: Swahili Wisdom
Dalili za Mvua ni Mawingu!
Kabla jambo lolote halijatokea huwa kuna dalili zinazotangulia kuashiria matukio fulani. Dalili hizo zikijitokeza humuandaa muhusika kujiweka tayari kulipokea jambo litakalotokea kwa umakini zaidi.
Baada ya Dhiki Faraja
Tunakumbushwa kuwa kila wakati mgumu ambao mtu anapitia utapita na baadaye utakuja wakati wa raha ambao utamfanya kusahau magumu yote aliyopitia. Inasemekana kuwa mara nyingi magumu tunayopitia ni dalili ya kupata faraja huko mbele. Tunafundishwa kutokata tamaa kutokana na magumu tupitiayo badala yake tufanye kazi kwa bidii katika mazingira yoyote kwani baadaye matunda mazuri yataonekana
Pilipili Usizozila Zakuwashia Nini?
Ni fundisho kwa wale wanaopenda kuwachunguza wenzao kwa mambo ambayo hayawahusu hasa wambea wenye tabia za kuchonganisha watu kwenye jamii, leo atachukua la Hadija atampelekea Zuena kesho anachukua la Maria atampelekea Subira.
Mgaagaa na Upwa Hali Wali Mkavu
Mtu yeyote anayehangaika na shughuli mbali mbali au mtu mwenye bidii za kazi huwa hakosi mafanikio au matokeo mazuri, hupata riziki, mafanikio/matokeo mazuri ambayo humfariji na hali kadhalika huyafurahia hapo mbeleni.
Kidole Kimoja Hakivunji Chawa
Msemo huu unasisitiza umuhimu wa watu kushirikiana katika maisha ya kila siku. Ushirikiano ni jambo la msingi katika kufanikisha jambo lolote. Kufanya mambo bila ushirikiano kunaweza kukasababisha hali kuwa ngumu na hatimaye mafanikio yanaweza kuwa madogo.
Kuishi Kwingi Kuona Mengi
Maisha tunayoishi ni mchakato wenye taarifa nyingi (mbaya na nzuri) ili uweze kuishi maisha marefu na uone mengi ni kumtegemea Mungu ili uweze kuzichakata taarifa vizuri ktk maisha yako yote.
Haba na Haba Hujaza Kibaba
Usikate tamaa unapoanza na kidogo ulichonacho hicho ndiyo kitakuwa ufunguo wa mafanikio yako. Kwa mfano unaanza biashara na pesa kidogo mathalan shilingi elfu ishirini, usiidharau, hiyo hiyo elfu ishirini uliyoanza nayo baada ya mwezi mmoja unaweza kujikuta una laki moja. Tuwe na moyo wa subira na moyo wa kuthubutu. Pia msemo huu unafanana na uleContinue reading “Haba na Haba Hujaza Kibaba”
Simba Mwenda Pole Ndie Mla Nyama
Tuaona simba awindapo anakuwa makini na anatumia juhudi na maarifa ili apate mawindo yake. Hii ina maana kuwa katika maisha lazima uwe na malengo na si hivyo tu, ili kufanikiwa ni lazima uwe na juhudi na umakini mwingi unahitajika. Inabidi utumie busara na maarifa katika kuyafikia malengo yako. Ukizingatia hayo, utafanikiwa, tuache uvivu.
Ukitaka cha Uvunguni Sharti Uiname
Mafanikio katika maisha yetu ni kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Chochote unachokitaka lazima juhudi yako itumike ili uone matunda yake.