Maisha yanafananishwa na muendesha baiskeli. Maisha yanaendeshwa na nguvu zako mwenyewe, hakuna mafuta yanayotumika. Hivyo nguvu zako ndio mafuta yenyewe.
Tag Archives: Swahili Wisdom
“Malezi Ruksa” Yana Athari Kwa Watoto
Malezi Ruksa (Permissive Parenting) ni aina mojawapo ya malezi ambayo mtoto anapewa ruksa ya kufanya au kuchagua chochote anachopenda/anachotaka bila ya kudhibitiwa. Malezi haya humpa mtoto uhuru uliopitiliza kiasi kwamba mtoto anasahau wajibu wake. Hata hivyo, hii ni aina ya malezi inayomfanya mzazi ajione anampenda sana mtoto wake.
Huwezi Kusukuma Gari Bovu Ukiwa Umekaa Ndani Yake
Gari ni aina ya chombo cha usafiri kinachoendeshwa kwa kutumia nishati ya mafuta na gesi. Dereva ndiye analiendesha na kulitunza gari. Endapo likipata hitilafu yeyote ile, dereva ndiye atakayelazimika kuteremka chini na kulikagua. Pale atakapogundua kama kuna hitilafu yoyote, ni wajibu wa dereva kutafuta mafundi wa kutatua tatizo hilo kwa kuwa wanayo maarifa ya kutosha.
Kuishi Kwingi Kuona Mengi
Kuishi ni neno linalotokana na maisha. Maisha ni siku au miaka tunayojaliwa na Muumba wetu baada ya kuzaliwa. Wenzetu wa zamani waliishi miaka mingi sana, wengine miaka 700 mpaka 900. Nyakati hizi tulizo nazo kuishi kwingi ni miaka 100 tu tena ni kwa wachache sana. Kuishi kwingi na kuona mengi hapa anazungumziwa mtu aliyeishi miaka 50 au 60.
Fuata Maadili Uishi Kwa Amani
Amani ni kitu cha msingi sana katika maisha. Unaweza kuwa na kila kitu katika maisha yako lakini ukikosa amani moyoni mwako, yote yanakuwa ni kazi bure.
Tuwapende Ama Tuwachukie Watu Kwa Kadri
Kupendana ni jambo la heri na la kupendeza sana.Hata maandiko yanatuasa tupendane. Lakini inabidi tuwe makini katika hilo maana huyo huyo umpendae anaweza kukugeuka siku yoyote. Hapo unaweza hata kujutia ulichokuwa umemfanyia huko nyuma. Uzoefu pia unaonyesha kuwa unaweza ukamchukia sana mtu lakini baadaye akaja kuwa wa msaada sana kwako siku ukipata shida.
Duniani Kuna Watu Waliondaliwa Maisha Na Wanaojiandalia Maisha
Msemo huu unazungumzia uhalisia wa maisha katika dunia hii tunayoishi. Wako watu wanaishi kutokana na hali ya wale waliowatangulia. Kama wazazi au walezi walikuwa na jina la kusifika, basi kizazi kinachofuata kitatembea katika hali ile ile. Kwa mantiki hii,?watakuwa wepesi kuonekana katika eneo lolote lile kutokana na majina makubwa wanayotembea nayo. Mfano kwenye siasa watoto wa wenye majina ni rahisi kufikiriwa na kupata kile wanachokitaka, pamoja na kazi nzuri, kisa tu, jina kubwa linawalinda.
Kushindwa Ni Sehemu Ya Maisha
Wengi wetu katika maisha, kuna mambo ambayo huwa tunapanga kuyafanya. Unaweza kupanga kwa muda wa dakika tano au kumi, inategemea, haijalishi. Kwa mfano, mtu akienda shule mpaka chuo, kwa kawaida anategemea kuwa akimaliza masomo yake atakuwa mtu mkubwa na mwenye nafasi katika jamii yake.
Akumulikaye Mchana Usiku Hukuchoma
Maadam tunaishi hapa duniani, tunakutana na marafiki wazuri, wabaya, wanafki, wambea na wengine wengi tu. Kwa mfano, rafiki yako unayemwamini sana anaweza kukutania, kukutishia au kukusema vibaya hadharani, yaani waziwazi, lakini kwa kuwa ni rafiki yako mmeshibana, unaona ni utani au kawaida tu, na unaweza ukamchukulia poa.
La Kuvunda Halina Ubani
Katika maisha ya ndoa kuna misukosuko mingi. Mingine inavumilika na mingine haivumiliki. Ninachotaka kusema hapa ni kwamba katika kupendana kwa nyie wawili mara nyingi si nyote wawili mnakuwa mnapendana kwa dhati, yaani kupendana kwa hali na mali.