Ni fundisho kwa wale wanaopenda kuwachunguza wenzao kwa mambo ambayo hayawahusu hasa wambea wenye tabia za kuchonganisha watu kwenye jamii, leo atachukua la Hadija atampelekea Zuena kesho anachukua la Maria atampelekea Subira.
Tag Archives: Sonona
Mgaagaa na Upwa Hali Wali Mkavu
Mtu yeyote anayehangaika na shughuli mbali mbali au mtu mwenye bidii za kazi huwa hakosi mafanikio au matokeo mazuri, hupata riziki, mafanikio/matokeo mazuri ambayo humfariji na hali kadhalika huyafurahia hapo mbeleni.
Kidole Kimoja Hakivunji Chawa
Msemo huu unasisitiza umuhimu wa watu kushirikiana katika maisha ya kila siku. Ushirikiano ni jambo la msingi katika kufanikisha jambo lolote. Kufanya mambo bila ushirikiano kunaweza kukasababisha hali kuwa ngumu na hatimaye mafanikio yanaweza kuwa madogo.
Kuishi Kwingi Kuona Mengi
Maisha tunayoishi ni mchakato wenye taarifa nyingi (mbaya na nzuri) ili uweze kuishi maisha marefu na uone mengi ni kumtegemea Mungu ili uweze kuzichakata taarifa vizuri ktk maisha yako yote.
Haba na Haba Hujaza Kibaba
Usikate tamaa unapoanza na kidogo ulichonacho hicho ndiyo kitakuwa ufunguo wa mafanikio yako. Kwa mfano unaanza biashara na pesa kidogo mathalan shilingi elfu ishirini, usiidharau, hiyo hiyo elfu ishirini uliyoanza nayo baada ya mwezi mmoja unaweza kujikuta una laki moja. Tuwe na moyo wa subira na moyo wa kuthubutu. Pia msemo huu unafanana na uleContinue reading “Haba na Haba Hujaza Kibaba”
Simba Mwenda Pole Ndie Mla Nyama
Tuaona simba awindapo anakuwa makini na anatumia juhudi na maarifa ili apate mawindo yake. Hii ina maana kuwa katika maisha lazima uwe na malengo na si hivyo tu, ili kufanikiwa ni lazima uwe na juhudi na umakini mwingi unahitajika. Inabidi utumie busara na maarifa katika kuyafikia malengo yako. Ukizingatia hayo, utafanikiwa, tuache uvivu.
Ukitaka cha Uvunguni Sharti Uiname
Mafanikio katika maisha yetu ni kujituma na kufanya kazi kwa bidii. Chochote unachokitaka lazima juhudi yako itumike ili uone matunda yake.
MAHUSIANO MAZURI YANAYO RUHUSU MAJADILIANO
Mama Sixtha Komba (M&E Officer, TEWWY) atuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na uwanja wa majadiliano hasa kati ya vizazi.
BUSARA ZIANGUKIAZO KWENYE “T” TATU
Mama Sixtha Komba anatueleza juu ya T tatu ambazo unaweza tumia katika kuyakabili matatizo ukutananayo. Akianza na fafanuzi juu ya T tatu. T1 ni Tatizo T2 ni Tatuzi T3 ni Tokeo Mama Sixtha Komba anaendelea kufafanua hizi T tatu katika nyanja mbili, hasi na chanya kwa kutumia mfano wa mwanafunzi aliyefeli mitihani yake na jinsiContinue reading “BUSARA ZIANGUKIAZO KWENYE “T” TATU”