Chuya ni mpunga ambao unakuwa umejichanganya na mchele mzuri ambao upo tayari kwa kupikwa. Hizo chuya huwa zinatakiwa kuchaguliwa ili kupata mchele mzuri, tayari kwa kupikwa. Lakini inawezekana kwa watu wengine ambao ni wavivu, kuupika mchele ukiwa hivyo haujachaguliwa wasione tofauti ama vibaya.
Tag Archives: Mental Health
Furaha Ni Kama Marashi Kwani Huongeza Maisha
Wahenga wa kale walisema, “Kitu furaha ni sawasawa na marashi”, kwani huwezi kujipulizia wengine wasisikie harufu yake. Hii inajidhihirisha wazi kwamba ukiwa na furaha huwezi kuificha kwani mtu yeyote atakayekuona atatambua kuwa umefurahi au una furaha. Basi, endapo wewe umefurahi, jitahidi na watu wengine nao wafurahi kutokana na furaha yako.
Usitegemee Uzuri Wako Maana Kuna Siku Utazeeka
Wako mabinti zetu wengi ambao wanajiona ni wazuri kwa umbo na sura. Watu hao mara nyingi hujiona kuwa ni bora zaidi kuliko wengine. Na huwa wanapenda hata kuchagua ni nani watakuwa wenzi wao.
Anayekukosoa, Anakujenga!
Ni kawaida ya watu wengi kupenda kuonekana kuwa wako mbele sana katika kila jambo wanalolifanya. Hakuna mtu anayetaka kuonekana kuwa hawezi.
Mpe Adui Yako Tabasamu Badala Ya Machozi
Unaporuhusu uchungu na maumivu ndani yako ni rahisi sana kuchoka na kukataa tamaa. Usibebe kila kitu, na wala usichukulie kila kitu kwa uzito, utaelemewa.
Kubali Kupoteza Ili Uende Viwango Vingine
Katika maisha unaweza kupoteza nafasi, au watu uliowaamini sana. Pengine hata uliweza kufikiri kuwa bila wao maisha au malengo yako hayatafanikiwa.
Maisha Ni Kutegemeana
Maisha ya mtu ni fumbo zito. Kila mtu ana umuhimu katika maisha ya mwenzake. Hii ni kwa sababu maisha ni kutegemeana.
Wakati Mwingine Hawakupendi, Wanakupenda Kwa Kile Ulicho Nacho
Ni ukweli usiopingika kuwa watu humpenda mtu mwenye nacho. Watu wa aina hii, yaani wale wenye nacho, huwa na marafiki wengi kupita maelezo. Ukweli huu huonekana zaidi kama huyo mtu atakuwa ni mtoaji sana na ambaye anapenda kusaidia watu.
Heri Shetani Unayemjua, Kuliko Malaika Usiyemjua
Tupo duniani tukizungukwa na watu mbalimbali na wenye tabia tofauti tofauti. Tunaishi kwa kutegemeana maana sisi ni wanadamu ndiyo maana utaona watu wanasaidina kwa shida na raha. Zaidi ya hapo utaona kwenye jamii zetu, kuna watu wanaishi kwa kupendana kama ndugu na kufanya vitu pamoja na kushauriana kwa kila jambo linalokuja mbele zao.
Jielewe Kwanza Mwenyewe, Watakuelewa Pia
Kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa hata na vizazi vijavyo, hakikisha unajisoma na kujielewa mwenyewe, kwanza kwa mawazo yako na ujumbe wako. Ila kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa leo na baadae kusahauliwa, basi endelea kutafuta kueleweka na watu wa leo.