Lawama ni hali ya kulalamika kuhusu jambo ama tatizo fulani. Fedheha maana yake ni aibu. Mara nyingi watu hutumia muda wao mwingi kulalamikia ugumu wa maisha. Ukiwachunguza watu hao kwa undani utakuta ni wale ambao ni wavivu, wasiopenda kufanya kazi. Mara nyingi watu hao hushinda vijiweni na kuzungumza mambo ya umbea ambayo hayana tija kwao wala kwa jamii. Kati ya watu hawa huwa na dharau na kebehi, wasiotafuta fursa, wasiopenda kushirikiana na wenzao na wenye mtizamo hasi dhidi ya wenzao na wao wenyewe.
Tag Archives: Community
Mawazo Ya Watu Wenye Hekima Ni Kama Shamba
Hekima ni mojawapo ya vipaji ambavyo Muumba wetu hutoa kwa viumbe wake. Ieleweke kuwa, sio kila mtu anajaliwa kupata vipaji. Lakini endapo itatokea kuwa unataka kipaji basi unashauriwa kuwa ni vema ukaomba hekima.
Ziba Mwanya Usiruhusu Panya Kupita
Mwanya ni nafasi yoyote ambayo mtu au kitu kinaweza kupita au kupenyeza bila kizuizi. Unaweza kuwa mwanya mkubwa au mwanya mdogo, alimradi hauzuii kilichokusudiwa kupenyeza. Hii ina maana kuwa, jambo lolote linapoanza kuharibika, huanza kidogo kidogo au taratibu sana na wakati mwingine bila hata kutambua.
Mwongo Huwa Hasemi Yake
Mtu mwongo ni yule mtu ambaye anapenda kuongea mambo ya wenzake kwa ushabiki. Mara nyingi huwa anaongea katika mithili ya kumdhalilisha mtu. Watu wa aina hii huwa wana asili ya kuwa na marafiki wengi ambao huvutiwa na stori zake za uongo. Huo ni ubinadamu wa watu ambao hawajitambui. Mara nyingi, kinachofanyika hapo huwa ni unafiki mtupu.
Muda Haumsubiri Mvivu
Kila jambo lina wakati na majira yake. Hata tunapopanga mipango tunaweka na muda wa kutekeleza. Pamoja na hayo, inategemea na jinsi wewe mpangaji wa mipango kama unajali muda na wakati wa kuitekeleza. Usipozingatia utakuta muda umeondoka bila ya matokeo.
Akufaaye Kwa Dhiki Ndiye Rafiki
Kulikuwa na bawana mmoja ambaye alitaka kujua rafiki yake wa kweli ni nani. Siku moja alimwambia mkewe, “Mke wangu andaa chakula kizuri na kingi. Nataka kula na rafiki zangu wapenzi”. Mkewe alifanya kama alivyoamriwa na mumewe. Akanunua kila aina ya mapochopocho na kupika. Pia alinunua vinywaji vingi vya kutosha kwa ajili ya wageni wake.
Tafuta Raha, Shida Zinakuja Zenyewe
Neno shida lina maana pana sana. Tunaweza kusema kuwa shida ni tatizo ambalo mtu anakuwa nalo. Mtu anaweza asijue namna ya kujinasua au namna ya kufanya ili aondokane nayo.
Usiogope Kuchukiwa, Ogopa Kulaumiwa
Chuki na lawama ni mambo ambayo yanakuja kwa kasi sana katika maisha ya jamii zetu. Mbaya zaidi, katika mahali pa kazi, hayo yameanza kuwa ndio maisha ya wengi. Kwenye sehemu ya kazi, chuki huja kuhusiana na utendaji wa kazi wa mtu. Kuna ambaye anachukiwa tu kwa sababu ya utendaji wake wa kazi na umakini katika kuitenda kazi aliyokabidhiwa na mkuu wake wa kazi.
Hakuna Marefu Yasiyokuwa Na Ncha
Maisha ni mzunguko, na sisi binadamu tunapoishi hapa duniani, tunakutana na mambo mengi sana yakiwemo mazuri na mengine mabaya, ya kusikitisha na hata yanayofurahisha.
Ukubwa Ni Jaa
Jaa ni jalala, mahali ambapo watu hutupa taka taka zao. Kwa hiyo mtu mkubwa ni kama jaa, kila mwenye takataka zake, (matusi, lawama, n.k) humtupia yeye.