Matumizi Ya Teknolojia Ya Simu Yaleta Msaada Kwa Mama Na Mtoto

Katika kufanya kazi zake, “TEWWY” (Tap Elderly Women’s Wisdom for Youth), haiko mbali na kauli mbiu ya Kimataifa na Kitaifa ya Siku ya Wanawake Duniani 2023. Kauli mbiu hiyo ya “Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia, Chachu kuleta Usawa wa Kijinsia

Maji Ya Moto Hayaunguzi Nyumba

Maji ya moto katika usemi huu, tunamaanisha maneno maneno hayavunji mfupa. Ni kawaida kabisa kila siku iendayo kwa Mungu sisi binadamu, muda mwingi tunautumia kwa kusemana semana na kufanyiana vurugu nyingi za hapa na pale. Hata pale inapoonekana kuwa mtu anajihangaisha bila kuchoka ili kujitafutia riziki yake, vimaneno maneno huwa ni vingi sana

Ukomo Wa Subira Yako Ndio Mwanzo Wa Husuda

Kila jambo linalofanywa na mtu yeyote lina mahali pa kuanzia. Katika kuanza jambo kunahitajika mipango thabiti ili liweze kutekelezeka. Utekelezaji wa mipango hiyo, utahusisha binadamu wengine kwa asilimia kubwa. Kwa kawaida, kipindi hicho huwa ni cha mpito

Acha Kuishi Kwa Wasiwasi, Hapo Ulipo Bado Una Nafasi

Maisha ni kupanda na kushuka. Chochote utakachokifanya, ni lazima utapitia changamoto za aina mbali mbali. Changamoto hizo zisikufanye uishi kwa wasiwasi na pia zisikukatishe tamaa.

Tutumie Mikakati Thabithi Katika Kuwafunza Watoto Wetu Maadili Mema

Hapo zamani kulikuwa na kaka mmoja ambaye alikuwa akiwalea dada zake wawili. Aliwapenda sana na akawa karibu nao. Aliwalea vizuri na kuwapatia mahitaji yao ya msingi

Mtoto Umleavyo Ndivyo Akuavyo

Mithali hii ni ya msingi sana, kuanzia pale mtoto anapozaliwa kwani tabia ya mtu inaweza kuwa nzuri au mbaya kutegemea na alivyolelewa na kukuzwa. Mfano, kama baba anakuwa na tabia ya kufokafoka na ukali uliopitiliza kila anaporudi nyumbani, watoto wake huishi kwa kuogopa muda wao wote. Pia wanaweza wakajenga tabia ya kuwa na hofu kila wakati wanapomuona baba yao. Woga ukiwazidi pia huwafanya watoto kuwa na tabia ya uongo na hata ya unafiki. Watoto wana akili sana. Wanaweza wakaamua kuwa vile mzazi wanavyomuona anataka wawe

Mtandao Ni Uwanja Wa Ulaghai

Baadhi ya wasichana wamekuwa wakirubuniwa na baadhi ya wanaume wanaoishi nchi za nje. Warubuni na warubuniwa, hukutana kwenye mitandao ya kijamii. Utandawazi ndio chanzo kikubwa cha kuleta yote haya. Mahusiano huanzia hapo, kwenye mitandao, juu kwa juu