
Christina Mande
Wisdom&Wellness Counselor
Kizinga, Dar-es-Salaam
Katika familia, kama baba na mama wanagombana kila wakati, watoto ndio wanaoteseka kwa kukosa huduma za msingi hasa kama itatokea baba na mama wanatengana/kuachana.
Pamoja Tunaweza Kutiana Moyo kwa Mafanikio
Christina Mande
Wisdom&Wellness Counselor
Kizinga, Dar-es-Salaam
Katika familia, kama baba na mama wanagombana kila wakati, watoto ndio wanaoteseka kwa kukosa huduma za msingi hasa kama itatokea baba na mama wanatengana/kuachana.
Grace Mshanga
Wisdom&Wellness Supervisor
Temeke & Ubungo,Dar-es-Salaam
Usemi huu huhamasisha kutunza utajiri. Ukipata utajiri uwe mwangalifu sana. Kwa mfano, inawezekana ulikuwa na mabasi ya abiria 10, mwisho ukapoteza kila kitu ukakosa hata baiskeli ya magurudumu mawili.
Rustica Tembele
Founder & CEO
Maana yake, kitu kizuri hakiihitaji matangazo, uzuri wake huonekana kwa uwazi, lakini kitu kibaya huhitaji kutangazwa na hutembezwa ili watu wakione.
Msemo huu unaweza kutumika pale mtu anapojigamba sana mbele za watu kuwa yeye ni wa hivi ama vile, lakini watu hawavioni hivyo anavyojigamba navyo bali wanamuona kama mtu wa kawaida tu.
Suzan Mwingira
Administrative Assistant
Msemo huu unamaana kwamba ni vema kuweka kumbukumbu za vitu vyako katika mahali pa usalama na katika mpangilio mzuri au kupangilia kazi zako kwa ufasaha zaidi ili kukuwezesha kujua, kutambua kwa urahisi mwenendo mzuri wa kazi zako au biashara yako.
Sakina Bushiri
Wisdom&Wellness Counselor
Pugu, Dar-es-Salaam
Hii hutumika kuhimiza watu kufanya kazi kwani kwa kufanya hivyo hutolala njaa. Katika mfano huu, mvuvi hali chakula bila mboga.
Christina Mande
Wisdom&Wellness Counselor
Kizinga, Dar-es-Salaam
Ukimpenda mtu mpende na makandokando yake. Ina maana kuwa unapompenda mtu uwe tayari kupenda mazuri yake pamoja na yale ambayo hayakupendezi. Hali kadhalika, wapende ndugu zake na wa wale wote anaohusiana nao, usibague.
Grace Mshanga
Wisdom&Wellness Supervisor
Temeke & Ubungo,Dar-es-Salaam
Hii huwafundisha na kuwaweka tayari wanandoa wapya kuwa hata tatizo liwe kubwa na limedumu kwa muda kiasi gani, mwisho wake ni kusamehana na kuishi kwa furaha na amani kama mwanzo.
Grace Mshanga
Wisdom&Wellness Supervisor
Temeke & Ubungo,Dar-es-Salaam
Katika hali ya kawaida binadamu kufanya kazi ni adha lakini mapato yapatikanapo ni kicheko. Hivyo vijana na wana ndoa wapya huhamasishwa kufanya kazi kwa bidii ili kupata mavuno bora na mengi ili kujitunza wenyewe na familia zao.
Paulina Ngwawasya
Wisdom&Wellness Supervisor
Ilala & Kinondoni, Dar-es-Salaam
Mwanadamu peke yako huwezi kufanikisha malengo yako katika maisha kwa kujitenga, unahitaji ushirikiano. Pia ina maana kwamba ushirikiano katika jamii ni muhimu sana kwani ushirikiano huleta maendeleo na mafanikio mazuri katika jamii au kazi. Msemo huu unatukumbusha kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa.
Sakina Bushiri
Wisdom&Wellness Counselor
Mangaya, Dar-es-Salaam
Usemi huu hutumika kuwaasa watu wasiopenda kufuata/kusikiliza wanayoambiwa na wakubwa; kwani mwishowe hufikwa na matatizo wakajuta.