Tuchukue Tahadhari Stahiki, Dunia Inabadilika Kwa Kasi Mno

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Ni ukweli usiopingika kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa sana kila kukicha, mithili ya mtu aliyegeuza miguu juu, kichwa chini. Dunia ya leo siyo kama ile ya zamani. Dunia ya sasa imekuwa na mambo mengi ya aibu, maovu ya kutisha na ya kusikitisha kiasi kwamba ubinadamu au utu umetoweka. Imefika mahali hatuna huruma tena, tumekuwa kama wanyama. Mambo mengi mabaya yanaibuka kila siku na hata usalama wa binadamu upo mashakani.

Baadhi ya mifano inayoonyesha kuwa dunia inababadilika kwa kasi ni hii ifuatayo: vita kati ya nchi na nchi, wivu wa kimapenzi, mahusiano mabaya kati ya vijana na vijana, wazazi na wazazi, magomvi, roho ya kwa nini, kinyongo, usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya, utumwa wa ngono, ushirikina na hata vifo vitokanavyo na kuuana. Mengine ni familia kuwatesa na kuwanyanyasa watoto wao wenyewe huku watoto wadogo wakilawitiwa na kubakwa hata na wazazi wao wenyewe> Watoto wamekuwa in wahanga wa maisha yao kwani hawawezi kijitetea. Hali inatisha kwani haingii kichwani unapomuona mzazi anamlawiti mtoto wake mwenyewe wa kumzaa. Dunia inakwenda wapi? Utu uko wapi? Tunatamani dunia isimame ii tusioweza kuendana na spidi yake hiyo. tuweze kuteremka.

Yote hayo yamebebwa ndani ya methali inayosema, “Dunia ni tambara bovu” huku amani furaha na upendo vikitoweka na ghasia zilkisheeni.

Simulizi hii inatukumbusha kuwa makini na matukio yanayotokea duniani na kututaka tuchukue tahadhari stahiki na madhubuti. Tukishindwa kufanya hivyo, tunaweza kuendelea kubakia kwenye ile dunia ambayo ni tambara bovu.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Maisha Mashenzi

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Maisha ni zawadi ambayo Mungu ametupa wanadamu ili tuishi kwa mafanikio kadiri alivyotuahidi maana vyote chini ya jua ni vyetu kwa hiyo kila mtu awe na maisha mazuri na yenye baraka.

Katika maisha yetu ya kila siku toka tuzaliwe hadi leo, tumeshuhudia mambo mengi kutoka kwa marafiki zetu, majirani zetu, wafanyakazi wenzetu na hata kutoka kwa ndugu zetu wa kwenye koo zetu, jinsi watu wanavyoendesha maisha yao. 

Msemo wa maisha ni mshenzi, umenigusa sana. Ukichunguza kwa undani, utaona watu wengi wapo kwenye kasi ya ajabu ya kushindana nani ni zaidi ya mwenzie. Tukiwa kwenye nani zaidi ya mwingine, ndipo tunaona kuwa yule aliyetupa vyote, mwenye mamlaka na maisha yetu yote, tunamsahau. Huyu si mwingine bali ni Mungu ambaye ni Muumba wetu. Mara nyingi, tunajikuta tunaingia kwenye kutafuta mbinu nyingine za mkato ambazo zinaweza kukubeba juu kwa juu mpaka ukajiona wewe ni zaidi hakuna mwingine zaidi yako. Hali hii tumeishuhudia mara nyingi. Mathalani, fulani alikuwa na pesa nyingi, kwa maana ya kuwa alikuwa tajiri sana. Mwisho wake anakuwa masikini kupindukia. Hivyo, inabakia kuwa ni historia iliyobeba maumivu yenye fedheha kubwa. 

Maoni yangu ni kwamba tujitahidi kutafuta maisha mazuri yenye mafanikio kwa njia iliyo halali. Tukifanya hivyo, maisha yetu yatakuwa na baraka kutoka kwa Muumba wetu. Maisha mashenzi ni yale maisha ambayo unayaishi kinyume na mapenzi ya Mungu. Mwsho wake, unaishia kupata aibu na fedheha ambayo inaweza kudumu mpaka kwenye uzao wako.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Penye Mafanikio Kuna Furaha

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Shughuli yoyote ambayo mwanadamu anafanya ni kwa madhumuni ya kufanikiwa. Katika mafanikio hayo ndipo inazaliwa furaha. Daima ukiona mtu amefurahi sana, ukitafuta sababu utakuta kuwa kuna mahali amefanikiwa. Nyumba yeyote ambayo imejaa upendo, basi elewa kuwa pale pana mafanikio kwa njia moja au nyingine.

Maisha yanaenda vizuri kwa mafanikio yaliyopo. Nyumba ya namna hii huwa haipungukiwi wageni. Tegemezi huwa ni wengi kuliko maelezo. Lakini siri kubwa ni mafanikio ya mtu mmoja ambaye amehangaika kufikia hapo alipo. 

Usemi huu unafanana na ule usemao mkono mtupu haulambwi. Kwa kawaida, nyumba isiyo na kitu huwa haipati wageni. Hali kadhalika, nyumba za aina hii, yaani ambazo hazina kitu, ugomvi huwa hauishi. Hii ina maana kuwa huzuni na uchungu ndivyo vinakuwa vinatawala nyumba. Ikumbukwe kuwa, mafanikio yanatokana na bidii iliyowekwa na mtu, na si vinginevyo. Kila mtu anapaswa kujitahidi sana kuhangaikia mafanikio yake.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Heri Lawama Kuliko Fedheha

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Lawama ni hali ya kulalamika kuhusu jambo ama tatizo fulani. Fedheha maana yake ni aibu. Mara nyingi watu hutumia muda wao mwingi kulalamikia ugumu wa maisha. Ukiwachunguza watu hao kwa undani utakuta ni wale ambao ni wavivu, wasiopenda kufanya kazi. Mara nyingi watu hao hushinda vijiweni na kuzungumza mambo ya umbea ambayo hayana tija kwao wala kwa jamii. Kati ya watu hawa huwa na dharau na kebehi, wasiotafuta fursa, wasiopenda kushirikiana na wenzao na wenye mtizamo hasi dhidi ya wenzao na wao wenyewe.

Ukweli ni kwamba, katika maisha yatupasa tuwe na msimamo na tuwe na maamuzi ya kufanya mambo tunayoyaamini, mambo yaliyo sahihi na yenye uhakika. Haitasaidia kuacha kufanya kabisa au kuhofia kuwa wabaya wako watakulaumu. 

Kulaumiwa kutakuwepo kila siku, hata ungefanyaje. Kama ukilaumiwa, malalamiko yao hayatakuwa na mashiko kwani jambo lako utakuwa umelifanya na cha msingi, litakuwa linaonekana.

Kwa wale wanaopenda kulalalamika na kusema maisha ni magumu na kulaumu wenzao, tunaweza kusema kuwa hawana busara. Kukaa na kuogopa kufanya shughuli zako kwa sababu zisizoeleweka vizuri, na za kubahatisha, hatma yake ni kupata aibu. 

Simulizi hii inatufundisha kuwa yatupasa kutenda  jambo unaloliamini na unalolijua. Hutakiwi kuogopa watu wengine watasemaje kuhusu wewe. Watu wana uhuru wa kusema wanachotaka, hiyo isikusumbue. 

Hali kadhalika,, tunafundishwa kuacha kulalamika kila wakati. Yatupasa tuache uvivu na umbea. Tujifunze kuwa wabunifu, tufanye kazi kwa bidii, tujitume na tutafute fursa mbalimbali katika maisha yetu. Maisha ni kujituma, maisha ni mapambano. Hakuna fedhea wala lawama katika kupambana na maisha.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Mawazo Ya Watu Wenye Hekima Ni Kama Shamba

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Hekima ni mojawapo ya vipaji ambavyo Muumba wetu hutoa kwa viumbe wake. Ieleweke kuwa, sio kila mtu anajaliwa kupata vipaji. Lakini endapo itatokea kuwa unataka kipaji basi unashauriwa kuwa ni vema ukaomba hekima.

Kwa kawaida, mtu mwenye hekima huwa ana busara sana. Mara nyingi watu wa aina hiyo, ambao wana hekima, ndio huwa wanakuwa viongozi katika familia zao. Uzoefu unaonyesha kuwa watu wenye hekima huwa na uwezo wa kutatua migogoro na matatizo katika jamii. Hali kadhalika, watu hawa huwa hawakubali kushindwa katika suala lolote. Pia huwa tayari kwa jambo lolote litakalokuja kutokea mbele yao. Watu wa namna hii ndio ambao hutumika na hufaa sana kwenye usuluhishi wa migogoro ya mashamba.

Ukiwa na hekima hakuna jambo litakukwaza. Busara zako na hekima ndizo ambazo zitakuongoza. Tunashauriwa kumwomba Mungu atupatie hekima kwa ajili ya kutuwezesha kuwasaidia watu wengi kwenye jamii zinazotuzunguka

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Ziba Mwanya Usiruhusu Panya Kupita

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Mwanya ni nafasi yoyote ambayo mtu au kitu kinaweza kupita au kupenyeza bila kizuizi. Unaweza kuwa mwanya mkubwa au mwanya mdogo, alimradi hauzuii kilichokusudiwa kupenyeza. Hii ina maana kuwa, jambo lolote linapoanza kuharibika, huanza kidogo kidogo au taratibu sana na wakati mwingine bila hata kutambua.

Kwa mfano, ukuta wa nyumba unapoanza kupasuka, huanza kidogo kidogo. Endapo hutachukua tahadhari kuuziba mwanya huo mapema, ni dhahiri kuwa utaishia kujenga ukuta wote kutokana na uharibifu mkubwa utakaokuwa umejitokeza.Kwa hiyo tunashauriwa kuwa, mara unapoona jambo lako linaanza kuharibika, hasa katika hatua za mwanzo, anza kudhibiti hali hiyo mapema ili kuepuka hasara au madhara yanayoweza kujitokeza baadaye.

Usemi huu unatufundisha kuwa makini mara tuonapo uharibifu unaanza kujitokea hata kama utakuwa ni mdogo kwa kiasi gani. Tusidharau, tujifunze kuwahi kurekebisha jambo mara linapotokea, ni muhimu sana kwa ajili ya kuepusha hasara, madhara na mambo mengine yanayoweza kutokea kutokana na uharibifu huo.

Kimsingi, tuepuke kudharau ama kutozitilia maanani, changamoto ndogo ndogo, bali tuhakikishe tunazitatua mapema ili kuepusha shari. Msemo huu unaendana na ule usemao, “Usipoziba Ufa, Utajenga Ukuta.” Sote tunajua kuwa kujenga ukuta ni gharama kubwa sana na ndio maana tunahimizwa kuchukua hatua mapema, mara tu tatizo linapotokea.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Mwongo Huwa Hasemi Yake

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Mtu mwongo ni yule mtu ambaye anapenda kuongea mambo ya wenzake kwa ushabiki. Mara nyingi huwa anaongea katika mithili ya kumdhalilisha mtu. Watu wa aina hii huwa wana asili ya kuwa na marafiki wengi ambao huvutiwa na stori zake za uongo. Huo ni ubinadamu wa watu ambao hawajitambui. Mara nyingi, kinachofanyika hapo huwa ni unafiki mtupu.

Alikuwepo kaka mmoja ambaye alikuwa anaishi na dadake pamoja na dada wa kazi nyumbani kwake. Dada wa kazi alikuwa anatoka kwenye familia ya mke wake. Kaka huyo pamoja na mke wake walijaliwa na Mungu watoto wawili. Baadae huyo kaka alipata uhamisho wa muda kwenda nje ya jiji la Dar es Salaam. Aliondoka peke yake bila familia yake. Familia yake ilibaki maana walikuwa wakiishi kwenye nyumba yao walioijenga.

Wakati mume anaondoka kwenda uhamishoni, mke wake alikuwa na mimba, lakini ilikuwa bado changa. Kwa bahati mbaya, mimba hiyo iliharibika. Lakini yule dada hakumwambia wifi yake yale yaliyomsibu. Badala yake alimwambia yule dada wa kazi. Kama tunavyojua, duniani hakuna siri ya watu wawili. Yule dada wa kazi alimtonya wifi mtu. Wifi mtu alikuja juu vibaya sana. Alimwambia kuwa hapaswi kumwambia dada wa kazi mambo mazito kama hayo. Aliendelea kwa kusema kuwa, mambo hayo angepaswa kumwambia yeye, ambaye ni wifi yake, na si vinginevyo. Hakuishia hapo kwani yule wifi alimfungulia risala ndefu na kumtukana matusi ya nguoni. Kama vile matusi hayakutosha, kilichofuatia ni kupeleka taarifa za uongo kwa kaka yake. Aliongeza na chumvi kwa kusema kuwa “Mke wako ni malaya sana na kwamba, anadiriki hata kuingiza wanaume ndani ya nyumba yenu ya ndoa.”

Kutokana na uzushi huo, ndoa ilianza kuyumba. Mume alianza kuwa na vituko vya ajabu kwa mke wake. Kwa kusema kweli, alikuwa haeleweki kabisa. Ni miaka mawili sasa mume haonekani nyumbani. Bahati nzuri mke alikuwa ni mtumishi wa umma, hivyo alikuwa anayamudu maisha yake. Yaani yale mabaya yote yaliyokuwa yakifanywa na dada mtu, yalikuwa yanageuzwa pale yanapofikishwa kwa kaka yake. Yalionekana ni mambo mabaya aiyokuwa akifanya wiki yake, yaani mke wa kaka yake.

Lakini, ikumbukwe kuwa Mungu hamfichi mnafiki. Ilitokea siku moja, jirani ambaye waliyekuwa wanapanga naye hayo mambo, nafsi ilimsuta. Aliona ni vema amweleze kila kitu, yaani ukweli wote. Alimweleza kuwa yale yote aliyokuwa akiambiwa na dada yake ni ya uongo mtupu. Aliendelea kwa kusema, “Umekuwa unamshutumu bure mkeo kwani yeye hafanyi hayo mambo machafu unayoelezwa, bali yeye na dada yake ndio huwa wanayafanya”. Hivyo alimsihi sana huyo kijana kutoamini mambo yoyote kutoka kwa dada yake, kwani yote yalikuwa ni uzushi mtupu.

Mume aiamini maneno ya yule mama. Kwa ghadhabu, alimfukuza dada yake pamoja na yule dada wa kazi kwani na yeye alikuwa na mchango mkubwa sana katika kuifarakanisha familia hiyo ambayo haina hatia. Uongo wao umewaumbua vibaya sana. Sasa hivi wamebaki wakiona haya sana na wanashindwa kumwangalia huyo kaka na mke wake. Wamebaki hawana hata mahali pa kuweka nyuso zao. Fundisho kuu hapa ni kuwa binadamu, yatupasa tuache uongo na tusipende kuwatungia wenzetu mambo mabaya kwani ipo siku unaweza kuja kuumbuka vibaya na kusutwa hadharani. Sidhani kama kuna mtu anayependa kuumbuliwa hadharani kwani ni aibu isiyoisha milele.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Muda Haumsubiri Mvivu

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kila jambo lina wakati na majira yake. Hata tunapopanga mipango tunaweka na muda wa kutekeleza. Pamoja na hayo, inategemea na jinsi wewe mpangaji wa mipango kama unajali muda na wakati wa kuitekeleza. Usipozingatia utakuta muda umeondoka bila ya matokeo.

Mara nyingi hayo huwa yanatokea kwa watu ambao ni wavivu. Mvivu mara nyingi huwa ni muongeaji na mpangaji mzuri lakini inapofika kwenye kutekeleza inakuwa ngumu. Zaidi, yeye huwa anasogeza ratiba mbele. Akisema hiki nitafanya kesho na hiki keshokutwa. Mwisho anajikuta anakwenda nje ya muda.

Kumbuka muda haumsubiri mtu, mwisho unajikuta una mipango isiyotekelezeka. Watu wa namna hii huwa wanalaumu watu kumbe tatizo liko kwao. Mvivu hana rafiki. Tujali muda ili kufanikisha shughuli zetu. Kazi billa mpangilio, hazina matunda mazuri.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Akufaaye Kwa Dhiki Ndiye Rafiki

Avelina Hokororo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Avelina Hokororo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kulikuwa na bawana mmoja ambaye alitaka kujua rafiki yake wa kweli ni nani. Siku moja alimwambia mkewe, “Mke wangu andaa chakula kizuri na kingi. Nataka kula na rafiki zangu wapenzi”. Mkewe alifanya kama alivyoamriwa na mumewe. Akanunua kila aina ya mapochopocho na kupika. Pia alinunua vinywaji vingi vya kutosha kwa ajili ya wageni wake.

Baada ya kumaliza kutayarisha kila kitu, alimwagiza mkewe aandae na kuweka mezani tayari, ili wageni wakifika waweze kukuta kila kitu kiko tayari. Hatimaye yule bwana akamwambia mkewe afunge mlango wakati yeye anaenda kuwaita wageni. Akatoka nje huku akipiga kelele ya kuomba msaada kuwa nyumba yake ilikuwa inaungua moto kule ndani.

Majirani wengi walibaki ndani kwao ila wapita njia na baadhi ya majirani wachache walikimbilia ndani kutoa msaada kutokanana na kilio chake. Yule bwana alifungua mlango watu wakaingia naye. Walipofika ndani walishangaa kuona kuwa hakukuwa na moto wowote, bali walikuta chakula mezani. Jambo la kufurahisha zaidi, walikaribishwa mezani ili waweze kushiriki karamu ile. Watu walikula na kusaza, wakamshukuru mwenyeji wao kabla ya kuondoka na kuelekea makwao.

Mkewe alimuuliza mume wake maana ya tukio hilo. Swali hili lilikuja baada ya mke wake kutowaona hao marafiki ambao alikuwa anawategemea na aliokuwa amewaandalia hicho chakula. Yeye alitegemea kuwaona hao wageni na majirani zake ambao walikuwa na mahusiano ya kiujirani. Badala yake walikuja watu ambao hakuwategemea kabisa maana walikuwa wengine mafundi wa gereji, wabeba mizigo na wapita njia tu. Mke kwa mshangao alimuuliza mume wake, “Hao ndiyo rafiki zako”?

Yule bwana akamjibu mke wake, “Ndiyo mke wangu hawa ndiyo rafiki zangu maana walinikimbilia kunipa msaada wa kuniokoa nilipolalamika kwamba nyumba yangu ilikuwa inaungua moto. Watu hawa bila kujali, waliacha shughuli zao wakaja haraka. Naamini ningesema kuna sherehe wangekuja wale ambao ulikuwa unawatarajia. Lakini nilisema ninaomba msaada waniokoe, ndiyo hawa wamekuja. Hawa ndiyo rafiki zangu wa ukweli”. Wahenga walinena, ‘Akufaaye kwa dhiki, ndiye rafiki’.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection 

Tafuta Raha, Shida Zinakuja Zenyewe

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Neno shida lina maana pana sana. Tunaweza kusema kuwa shida ni tatizo ambalo mtu anakuwa nalo. Mtu anaweza asijue namna ya kujinasua au namna ya kufanya ili aondokane nayo.

Ziko shida za aina nyingi, mathalani, shida ya kufiwa, kuuguliwa ama shida nyingine yoyote ile. Ukweli ni kwamba, shida halitafutwi bali inakuja tu bila ya taarifa ama mapatano. Mara nyingi shida huja wakati huna jinsi ya kutatua. Ndipo unapohitaji kusaidiwa ili utoke katika ile hali. Shida haina hodi kabisa nahivyo haingoji karibu.

Tukija kwenye eneo la raha, hapo lazima uitafute kwa namna yeyote ile. Lakini ieleweke kuwa, raha haiji kwa mtu anayependa kubweteka bweteka tu. Unapotafuta raha, utapambana kwa nguvu zako zote na namna zote ili uweze kufanikiwa. Kwa maana hiyo, bila kupambana, raha utaisikia kwa wenzio. Yakupasa uhangaike hapa na pale ili upate matokeo mazuri, upate kile ukitakacho.

Hii ni kusema kuwa, raha inatafutwa kwa udi na uvumba, lakini shida haitafutwi. Shida inakuja yenyewe bila kuitwa wakati raha inakuja kwa kutafutwa na inakuja kwa wakati na majira yanayoruhusiwa. Ndio maana wahenga walinena kua, ‘Mtaka cha Uvunguni Sharti Ainame”. Kamwe tusitegemee kuwa raha zitatufuata bila kuhangaika, hii ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa bidii zote.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

%d bloggers like this: