La Kuvunda Halina Ubani

Avelina Hokororo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Avelina Hokororo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kuvunda maana yake ni kitu chochote ambacho kimekaa muda mrefu na kinatoa harufu mbaya. Na ubani ni kitu kinachotoa harufu nzuri.

Continue reading “La Kuvunda Halina Ubani”

Usipime Umuhimu Wa Mtu Kwa Mahitaji Yako

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Binadamu kwa kawaida, tunaishi kwa kusaidiana. Inaweza ikatokea katika maisha yako ukawa na mtu ambaye kwako wewe ni msaada mkubwa. Pengine ni yeye anayekusaidia katika shida zako mbalimbali. Mtu huyo unaweza ukamuona kuwa ni rafiki au ndugu kwa sababu huwa ni kawaida yake kukusaidia siku zote. Kwa kifupi, mtu huyu tunaweza kusema kuwa ni mkombozi wako kwa kila hali. 

Kuna dada mmoja ambaye alikuwa na mazoea sana na mimi kiasi kwamba, kama akipata shida yoyote, huja kwangu bila wasiwasi wowote. Ikatokea siku moja alikuja kwangu lakini siku hiyo mimi sikuwa na nia ya kumtimizia matakwa yake. Hii ilitokana na sababu kwamba, alikuwa msumbufu sana wakati wa kurudisha. Kwa hali hiyo nilifikia mahali nikawa nimechoka. Kwa uwazi kabisa, nilimwambia kuwa sitaweza kumsaidia safari hii. Aliondoka akiwa na kinyongo moyoni mwake. 

Matokeo yake, alianza kunitangaza kuwa, kwanza sina chochote na wala sifai kwa lolote. Kisa tu eti nimekataa kumsaidia siku hiyo. Alianza kuniona kuwa sina umuhimu tena kwake. Alinisemea ovyo sana kwa watu. Lakini kwa waliokuwa wanamjua, na jinsi nilivyokuwa namsaidia mara kwa mara, walimuona hana shukurani. Waliweza kumwambia machoni pake kuwa hana fadhila na kwamba hakumbuki alikotoka. 

Usemi huu unatuasa tusipime umuhimu wa mtu kwa shida zetu. Ilikuwa ni dhahiri kabisa umuhimu wangu kwa dada huyu ulionekana kwake pale tu nilipokuwa namsaidia. Bila hivyo, bila kumpa misaada, alinigeuza kuwa mimi si lolote wala chochote kwake. Hiyo siyo sahihi hata kidogo. Umuhimu wa mtu haupimwi kwa misaada ama ufadhili anaokupatia. Tujifunze kuwa na shukrani kama binadamu kwani tunahitajiana. Kila mmoja wetu ana umuhimu wake.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Matumizi Ya Teknolojia Ya Simu Yaleta Msaada Kwa Mama Na Mtoto

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Katika kufanya kazi zake, “TEWWY” (Tap Elderly Women’s Wisdom for Youth), haiko mbali na kauli mbiu ya Kimataifa na Kitaifa ya Siku ya Wanawake Duniani 2023. Kauli mbiu hiyo ya “Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia, Chachu kuleta Usawa wa Kijinsia.” TEWWY inajitahidi kupunguza tofauti za kidigitali kati ya kizazi kipya na kizazi cha zamani kwa kutumia Teknolojia (simu) kutoa huduma kwa wanasihiwa wa jinsia zote.

Continue reading “Matumizi Ya Teknolojia Ya Simu Yaleta Msaada Kwa Mama Na Mtoto”

Maji Ya Moto Hayaunguzi Nyumba

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Maji ya moto katika usemi huu, tunamaanisha maneno maneno hayavunji mfupa. Ni kawaida kabisa kila siku iendayo kwa Mungu sisi binadamu, muda mwingi tunautumia kwa kusemana semana na kufanyiana vurugu nyingi za hapa na pale. Hata pale inapoonekana kuwa mtu anajihangaisha bila kuchoka ili kujitafutia riziki yake, vimaneno maneno huwa ni vingi sana.  

Haya yote hufanywa ili kumkatisha tamaa mhusika. Maneno yanayosemwa dhidi yako, mara nyingi huwa ni ya maudhi kiasi kwamba   yanaweza kukukatisha tamaa kabisa. Unaweza hata ukaacha kuendelea kuhangaika na shughuli zako za kimaendeleo.

Ushauri wangu ni kwamba, unatakiwa kuyapuuza maneno hayo kwa sababu hayakupunguzii chochote katika maisha yako. Kama ule usemi wa “Watasema mchana, usiku watalala”, kwenye hali hii, msemo huo una maana sana. Wewe kwa upande mwingine, utakuwa ukiendelea na shughuli zako kama kawaida. Wao wataendelea kubwabwaja wee mpaka wachoke.

Ndio maana ya usemi huu wa maji ya moto, pamoja na ukali wake hayawezi kuunguza nyumba. Hata watu waseme namna gani wewe utabaki vile ulivyo, sana sana wao ndio watapata taabu wakikuona kuwa hutetereki hata kidogo. Cha msingi, wewe endelea kujiamini na kutekeleza yale uliyoyapanga.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Tuwe Tayari Kufanya Kazi Wakati Wote

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kujitolea ni kufanya kazi bila kulipwa. Watu wengi hawajitolei kutokana na ukweli kwamba huwa hakuna malipo. Watu hupenda kulipwa hata kama kuna neno kujitolea limewekwa. Binadamu ndivyo tulivyo.

Continue reading “Tuwe Tayari Kufanya Kazi Wakati Wote”

Nyoka Na Jongoo

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Hapo zamani za kale, Nyoka alikuwa ana miguu lakini macho hakuwa nayo. Jongoo naye alikuwa na macho, lakini miguu alikuwa hana. 

Continue reading “Nyoka Na Jongoo”

Ukomo Wa Subira Yako Ndio Mwanzo Wa Husuda

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kila jambo linalofanywa na mtu yeyote lina mahali pa kuanzia. Katika kuanza jambo kunahitajika mipango thabiti ili liweze kutekelezeka. Utekelezaji wa mipango hiyo, utahusisha binadamu wengine kwa asilimia kubwa. Kwa kawaida, kipindi hicho huwa ni cha mpito. 

Continue reading “Ukomo Wa Subira Yako Ndio Mwanzo Wa Husuda”

Wazazi Wana Haki Ya Kutunzwa Na Watoto Wao

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kinachofuata ni kisa cha mama na mtoto wake wa kiume. Yaliyomo ndani ya kisa hiki yanaweza yakakuumiza sana kama una roho yenye huruma na ya kibinadamu.

Continue reading “Wazazi Wana Haki Ya Kutunzwa Na Watoto Wao”

Acha Kuishi Kwa Wasiwasi, Hapo Ulipo Bado Una Nafasi

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Maisha ni kupanda na kushuka. Chochote utakachokifanya, ni lazima utapitia changamoto za aina mbali mbali. Changamoto hizo zisikufanye uishi kwa wasiwasi na pia zisikukatishe tamaa.  

Continue reading “Acha Kuishi Kwa Wasiwasi, Hapo Ulipo Bado Una Nafasi”

Tutumie Mikakati Thabithi Katika Kuwafunza Watoto Wetu Maadili Mema

Grace Mshanga - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Grace Mshanga (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Hapo zamani kulikuwa na kaka mmoja ambaye alikuwa akiwalea dada zake wawili. Aliwapenda sana na akawa karibu nao. Aliwalea vizuri na kuwapatia mahitaji yao ya msingi. Kuhakikisha usalama wa dada zake, alijenga ukuta mrefu kuzunguka nyumba waliyokuwa wakiishi. Pia alihakikisha kuwa  milango ya nyumba ilikuwa imara kabisa. Kila siku jioni alifunga milango yote yeye mwenyewe. Baada ya kufunga milango, aliita majina ya dada zake wote ili kuhakikisha kuwa wapo chumbani kwao. Dada zake wakiitikia, anajiridhisha kuwa mambo ni shwari. 

Kujitaabisha kote huko ilikuwa ni kulinda heshima ya familia yao. Aliogopa kupata fedheha ya dada zake kupata mimba kabla ya kuolewa. Hakutaka kabisa aibu ya namna hiyo itokee.

Jitihada zake za ulinzi wa dada zake hazikuzaa matunda. Cha kushangaza, mmoja wa dada zake alipata kile alichokuwa hakitarajii kitokee. Alipata uja uzito. 

Kwa taharuki, kaka alichukua bunduki. Alitaka huyo dadake mjamzito amweleze imekuwaje mpaka ikawa hivyo. Dada yake naye bila kusita, alimjibu kaka yake  akasema, “kaka hili karavati kubwa kama la barabarani ulilojenga, lilingia hadi uani kwetu ili kutoa maji machafu. Kila siku jioni tulikua tunasafisha na maji safi na hapo ndipo mahali nilikua natokea kwenda kukutana na mvulana wangu. Nilikuwa narudi asubuhi sana kabla nyie hamjaamka”. 

Kaka alibaki mdomo wazi, ameduwaa asijue la kusema, wala la kufanya. Alifikiria jitihada zake alizozifanya za kuwalinda dada zake. Aliumizwa sana na hili tukio la dadake kupata mimba. Kwa hakika kufanya mambo bila mipango thabiti huwa hakuzai matunda. Kuzungushia ukuta mrefu kama wa magereza na kutengeneza milango imara hakukuwa suluhisho kwa kile alichokuwa akitaka kaka kisitokee kwa dada zake.

Tunajifunza nini kutoka simulizi hii? 

Tunajifunza umuhimu wa wazazi na walezi katika kuwalea watoto vizuri na kwa mikakati. Tukumbuke kuwa tunaishi na binadamu ambao kila moja ana akili zake. Kuzungushia ukuta peke yake bila kuwapa elimu ya kutosha ya namna ya kujitunza, haisaidii. Watoto wanapaswa kuambiwa bayana madhara yanayoweza kutokea wakijiingiza kwenye mapenzi katika umri mdogo. Muda zaidi utumike na wazazi/walezi katika kuwapa elimu kuliko kuzungushia ukuta mrefu ili kuwazuia watoto wasitoke nje ya geti. Watoto wanaweza kubuni njia mbalimbali za kujinasua kwenye vifungo wanavyopewa na wazazi/walezi wao. Watoto wanapaswa kufundishwa namna ya kuthamini utu wao na kwamba kila kitu kina wakati wake.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

%d bloggers like this: