Grace MshangaWisdom&Wellness Supervisor Temeke & Ubungo,Dar-es-Salaam Usemi huu huhamasisha kutunza utajiri. Ukipata utajiri uwe mwangalifu sana. Kwa mfano, inawezekana ulikuwa na mabasi ya abiria 10, mwisho ukapoteza kila kitu ukakosa hata baiskeli ya magurudumu mawili.
Category Archives: Wisdom&Wellness Talks
CHEMA CHAJIUZA, KIBAYA CHAJITEMBEZA
kitu kizuri hakiihitaji matangazo, uzuri wake huonekana kwa uwazi, lakini kitu kibaya huhitaji kutangazwa na hutembezwa ili watu wakione
MGAA GAA NA UPWA HALI WALI MKAVU
Sakina BushiriWisdom&Wellness Counselor Pugu, Dar-es-Salaam Hii hutumika kuhimiza watu kufanya kazi kwani kwa kufanya hivyo hutolala njaa. Katika mfano huu, mvuvi hali chakula bila mboga.
UKIPENDA BOGA, UPENDE NA MAUA YAKE
Christina MandeWisdom&Wellness Counselor Kizinga, Dar-es-Salaam Ukimpenda mtu mpende na makandokando yake. Ina maana kuwa unapompenda mtu uwe tayari kupenda mazuri yake pamoja na yale ambayo hayakupendezi. Hali kadhalika, wapende ndugu zake na wa wale wote anaohusiana nao, usibague.
HAKUNA NJIA NDEFU ISIYO NA MWISHO
Grace MshangaWisdom&Wellness Supervisor Temeke & Ubungo,Dar-es-Salaam Hii huwafundisha na kuwaweka tayari wanandoa wapya kuwa hata tatizo liwe kubwa na limedumu kwa muda kiasi gani, mwisho wake ni kusamehana na kuishi kwa furaha na amani kama mwanzo.
UNAPOFANYA KAZI NI ADHA TU, MAVUNO YAKIWA TAYARI NI VICHEKO
Grace MshangaWisdom&Wellness Supervisor Temeke & Ubungo,Dar-es-Salaam Katika hali ya kawaida binadamu kufanya kazi ni adha lakini mapato yapatikanapo ni kicheko. Hivyo vijana na wana ndoa wapya huhamasishwa kufanya kazi kwa bidii ili kupata mavuno bora na mengi ili kujitunza wenyewe na familia zao.