Jielewe Kwanza Mwenyewe, Watakuelewa Pia

Kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa hata na vizazi vijavyo, hakikisha unajisoma na kujielewa mwenyewe, kwanza kwa mawazo yako na ujumbe wako. Ila kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa leo na baadae kusahauliwa, basi endelea kutafuta kueleweka na watu wa leo.

Usitunze Huzuni Moyoni

Huzuni ni hali ya masikitiko yenye masononeko inayomfanya mtu akose furaha, amani na matumaini kwa kiwango kikubwa na kwa muda mrefu. Hali hiyo humfanya mtu atawaliwe na mawazo mengi sana, ikiwa pamoja na msongo wa mawazo na sonona. Inapokithiri bila kupata huduma sahihi huweza kusababishahta kifo.

Tuwe Wastaarabu Na Busara Katika Maongezi

Binadamu tunatakiwa kuishi kwa kufuata taratibu fulani zilizopo kwenye jamii, hii ni pamoja na jinsi tunavyozungumza na wenzetu. Kwa maana hiyo, ukiwa mstaarabu na mwenye busara huwezi kuuliza uliza watu maswali ambayo hayastahili kuulizwa, maswali kama: ‘Bado hujaolewa tu?….Una watoto wangapi?…Utazaa lini?…Mbona umri umeenda?…na mengine mengi.

Hekima Ni Jambo La Msingi

Kile unachokiita baraka au ushindi kilianza kama tatizo. Mara nyingi, yule anayefanikiwa kutatua matatizo huonekana kama ana baraka au mshindi fulani hivi. Ni kawaida kwa kila mwanadamu kupata matatizo. Pale mtu anapopata matatizo, ni vema kutafuta mbinu za kupambana nayo. Wengi hujaribu kukimbia matatizo yanapotokea.

Mafanikio Makubwa Yana Vikwazo

Njia nyepesi kabisa ya kutofika popote ni kusubiri ueleweke na kusifiwa na kila mtu kwa jambo uliloamua kulifanya. Uhalisia ni kwamba huwezi kueleweka kwa kila mtu na sio rahisi sana kusifiwa na kila mtu hasa jambo linapokuwa katika wazo ama hatua za awali.