Heri Shetani Unayemjua, Kuliko Malaika Usiyemjua

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Tupo duniani tukizungukwa na watu mbalimbali na wenye tabia tofauti tofauti. Tunaishi kwa kutegemeana maana sisi ni wanadamu ndiyo maana utaona watu wanasaidina kwa shida na raha. Zaidi ya hapo utaona kwenye jamii zetu, kuna watu wanaishi kwa kupendana kama ndugu na kufanya vitu pamoja na kushauriana kwa kila jambo linalokuja mbele zao.

Naamini tumeshuhudia hilo Mmakonde anakuwa na urafiki na Mchaga na wakaishi kwa upendo na kwa kushibana sana.

Unakuja wakati hali hiyo inabadilika. Utakuta majaribu yanajipenyeza na kuanza kuharibu umoja wao na kuanza kugombana na kutengana, na urafiki unavujika kwa lugha chafu na wakaanza kuonana kama maadui.

Ikifikia hali hiyo kila mtu anaenda upande wake na kuanza kutafuta rafiki mwingine ambae wataendana. Zaidi ya hapo tumeshuhudia wengi wakifikia maamuzi hayo, urafiki haudumu kwasababu uliyokuwa unayategemea yanakuwa sivyo. Mwisho unaanza kujilaumu na kusema, afadhali ningebaki na rafiki yangu wa awali.

Mara nyingi yanatukuta hayo kwa kukosa ufahamu wa kutambua kuwa wote ni binadamu na hakuna aliyekamilika. Jambo jepesi ni kuombana msamaha yaishe na mahusiano yaendelee. Mwisho inapelekea kumkumbuka uliyemwona shetani kuliko huyo uliyemuona malaika kwako.   

Kutokana na msemo huo nina ushauri kuwa dunia imejaa mapito, lakini msamaha na kuachilia, utaishi kwa amani ndani ya jamii. Mahusiano na watu wengine yatakuwa mazuri na uhakika wa kufanya mambo mbalimbali ya maendeleo, hayatakuwa magumu kwako.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Jielewe Kwanza Mwenyewe, Watakuelewa Pia

Victoria Nakajumo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Victoria Nakajumo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa hata na vizazi vijavyo, hakikisha unajisoma na kujielewa mwenyewe, kwanza kwa mawazo yako na ujumbe wako. Ila kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa leo na baadae kusahauliwa, basi endelea kutafuta kueleweka na watu wa leo. 

Kumbuka unaowasoma na kuwaelewa leo, jana na juzi hawakueleweka maana waliishi jana, wakiiwaza leo na wakaiandaa leo ili wewe wa leo usaidiwe na jana yao.

Je, unaamua kuwa kitabu cha kesho, unaielewa kesho au unataka uwafurahishe wasioiona kesho kwa kufuata mawazo yao badala ya yale Mungu kakupa kwa ajili yako na watu wake?

Sio vibaya kama utaeleweka leo, lakini lazima uanze kujielewa wewe kabla hawajakuelewa wengine.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection 

Usitumie Usomi Wako Kuwanyanyasa Na Kuwatambia Wenzako

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Wako watu wanaojiona, wanaojitapa na kutamba kuwa wana akili sana. Hujiona wamesoma na wameelimika zaidi ya wengine. Watu hawa huchukua fursa hiyo ya kuelimika kama fimbo ya kuwachapia wenzao. Huwanyanyasa wenzao kwani huwaona kuwa ni wajinga na pia hawana elimu. Hali kadhalika, huwadharau, kiasi kwamba hata kuongea nao inakuwa ni shida, kisa, eti hawajasoma.

Kujitamba na kujiona kuwa wewe umeelimika kuliko wengine ni kukosa hekima. Walioelimika, hawahitaji kujionyesha, kuringa, wala kujisifia sana kwani matendo na tabia njema, kauli nzuri, utulivu, hekima, busara, heshima na ukarimu ndivyo vitu vinavyomtambulisha mtu kuwa kuwa huyo ameelimika ipasavyo. 

Hapa tunakumbushwa kwamba kuelimika kwa mtu kunadhihirishwa na mahusiano mazuri na matendo mema katika jamii yake, jamii inayomzunguka.Hivyo, tunaaswa kuwa, tusiitumie elimu yetu kwa hasara, bali tuitumie kwa faida katika jamii zetu.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Mpatie Mtu Ujira Wake Kwa Wakati Anaostahili

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Kuna aina nyingi za ajira hapa duniani. Usemi huu unawalenga wale tunaowaajiri hasa kwenye kazi za nyumbani (house girls). Kuna tabia mbaya ya baadhi ya waajiri kwenye sekta hii kutokuwajali na kuwathamini wafanya kazi wa sekta hii.

Kuna mama mmoja alikuwa na dada wa kazi ambaye alikuwa amekaa naye kwa zaidi ya miezi sita bila kumlipa kile walichokuwa wamekubaliana. Kila wakati msichana akimuambia kuhusu malipo yake, yule mama humtukana na kumsimanga vibaya. Aliweza kudiriki hata kumwambia kuwa hela zake za mshahara, zinanunua chakula anachokula.  

Kilichokuja kutokea siku moja, binti aliamua kuondoka na vitu vya thamani mle ndani. Aliweza kubeba mpaka nguo za mama na za baba. Kibaya zaidi, alimuachia mtoto wake wa miaka mitano pale nyumbani na geti likiwa wazi.  

Mama aliporudi jioni alimkuta mtoto kachoka na kulia na alikuwa hajala kitu chochote. Kila akimuuliza mtoto alikuwa hawezi kusema. 

Roho mbaya ya mama, hayo yalikuwa ndio malipo yake. Hakuweza kumfuatilia maana alikuwa hajui alikuwa anatokea wapi. Wengi wa wasichana wa kazi tunawaokota hapa hapa mjini. Natumia neno ‘kuokota’ kwa sababu katika hali ya kawaida, palipo na upendo, ni lazima utapenda kufuatilia na kujua atokako. Kumbuka, yeye ni binadamu, likitokea la kutokea sijui utafanya nini?  

Ni tabia ya kiungu kumlipa yule anayekutumikia kwa wakati. Ndivyo ubinadamu unavyotakiwa kuwa. Isitoshe, huyo mfanya kazi wako amebeba maisha yenu wote humo ndani. Ana uwezo wa kufanya chochote kibaya anachotaka kwenu. 

Yatupasa tuheshimu kazi wanazofanya watumishi wa ndani. Ni vizuri tukawafanya kama sehemu ya familia zetu. Tunawahitaji sana, na kazi zao ni za msingi sana katika maisha ya mwanamke aliyeajiriwa. Hebu tubadilike kama tuna tabia mbaya za kunyanyasa wasichana wa kazi za ndani. Nao ni binadamu, wanahitaji upendo kama watoto wako.  

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Yatima Hadeki

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Neno yatima au ukiambiwa yule ni yatima kila mtu ataelewa. Yatima ni mtoto ambaye, aidha kafiwa na mzazi mmoja au kafiwa na wazazi wake wote wawili. 

Katika maisha yetu ya kila siku tunakumbana na yatima wengi. Hali kadhalika, tunashuhudia mambo mengi wanayopitia. Unaweza kukuta yatima wengine wanaishi vizuri lakini walio wengi wana changamoto za kusikitisha. Kuna kitu huwa kinaibuka kwa wengi wakishapitia hali hii ya uyatima. Mara nyingi wanakuwa na hali ya kutokujiamini na hivyo huanza kutegemea misaada kutoka kwa ndugu. Ikifikia hatua hiyo, ndipo tatizo huwa linaanza .      

Kuna mengi yanatokea katika mazingira haya. Huwepo ndugu ambao huonyesha kwamba wanachukua majukumu ya mzazi wao au wazazi wao. Hutokea kwamba majukumu wanayobeba huwa siyo sahihi. Hutokea uchu wa kutaka kudhulumu mali walizoachiwa na mzazi au wazazi. Mara nyingi, watoto hubaki wakinyanyasika na kukosa kabisa haki zao. Watoto wanakuwa hawawezi kuongea au kuuliza chochote kile kinacholetwa mbele ya macho yao. Hawawezi kudadisi kwa nini inakuwa hivyo. Pale inapotokea wanaletewa kitu,  wawe wanakipenda ama hawakipendi, watajijua wenyewe. 

Wakati mwingine watoto hutawanywa kwa lengo la kuwatenganisha na kupelekwa kule na huko, ili mradi tu wasiwe pamoja. Yote hiyo hufanywa ili tu mali za marehemu wazitumie wanavyopenda wao. 

Ukatili mkubwa wanaofanyiwa yatima, ni jambo ambalo linadhohofisha sana ustawi wa watoto kwenye jamii zetu.            

Tukiutafakari msemo huo hatuna budi kuliomba taifa liwaangalie yatima kwa jicho la pekee ili nao wawe na uhuru na haki ya kumiliki mali walizoachiwa na wazazi wao. Serikali iweke sheria za kuwabana ndugu ambao wanajiita ni wasimamizi wa mirathi ili wanapofikia hatua ya kugawa hizo mali wazipeleke mahakamani ili haki iweze kutendeka. 

Maoni yangu mengine ni kwamba yatupasa ndugu tuonyeshe upendo kwa yatima na kuwapa msaada pale unapohitajika maana hatujui kesho yetu. Hali hii itawapelekea yatima kuwa na amani na kuishi kwa furaha kama wanadamu wengine. Yatupasa tuwekeze kwa yatima ili na sisi watoto wetu watakapokuja kuwa yatima, waweze kupata msaada kutoka kwa watu wengine. Maisha ni mzunguko, na uyatima hauchagui wala haubagui. nyumba wala familia. 

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Usimtekenye Aliyekubeba, Atakudondosha

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Maisha yetu ni ya kutegemeana kwa kiwango kikubwa sana. Hakuna mtu atakayesema hapa alipo amefika kwa juhudi zake mwenyewe. Lazima kuna mahali alifika akakwama, na mtu mwingine akamkwamua na hatimaye akatoka.  

Mara nyingi, mtu anapata kazi kwa kusaidiwa na mtu mwingine. Lakini inafikia mahali mtu akishazoea kazi anaanza kujenga tabia ya kusahau. Hamkumbuki tena aliyemsaidia na kumfikisha hapo alipo. 

Kuna dada mmoja aliajiriwa na kampuni moja binafsi kwa msaada wa mtu. Yule dada baada ya kuzoea akawa anatembea na meneja wake. Cha kushangaza ni kuwa yule aliyemsaidia kupata kazi ni mke wa yule meneja wake. Binadamu ni kiumbe wa ajabu, hakawii kusahau. 

Baada ya muda mrefu wa kuwa na yule baba alifikia hatua ya kuanza kuwadharau na kuwanyanyasa wenzake pale kazini. Wenzake waliona isiwe taabu. Walichukua hatua ya kumueleza mhusika yaani mwenye mali yake, ambaye ni mke wake wa yule meneja. Walimweleza kila kitu.

Kilichotokea mke wa meneja aliamuru huyo dada afukuzwe kazi mara moja bila malipo yoyote. Maskini dada wa watu, ilibidi arudi zake mtaani kuhangaika. Usicheze na ’mali’ za watu, eh bwana. 

Sambamba na usemi huu ni ule usemao ukitaka kula na kipofu usimshike mkono. Binti alisahau kuwa pale alipelekwa na mtu, na siyo mtu tu bali ni mke wa meneja ambaye dada huyo aliamua iwe mali yake. Alikosea sana kuamua kumbeba mume wa watu bila kukukmbuka fadhila alizofanyiwa na huyo dada mwenye mume. Mungu hutoa malipo hapa hapa duniani. 

Ona sasa yaliyompata. Kwa kukosa heshima na fadhila kwa yule aliyemtafutia kazi, amerudi mtaani na kuendelea na mihangaiko yake. Maisha ni ya ajabu, hayana formula. Ukitenda mabaya kwa wenzio, malipo yake huwa ni hapa hapa duniani. 

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Barua Ya Moyo Husomwa Kwenye Paji La Uso

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Moyo ni kitu kidogo sana katika mwili wa mwanadamu. Moyo huwa hauonekani kwa jicho la kawaida, lakini moyo ndio uhai wa mtu ulipo. 

Moyo huwa unaongea pasipo kutamka neno. Moyo ukisimama hapo ndipo hata uhai wa mtu unakuwa umekoma. Moyo huua kwa fikira na kwa mawazo. Maamuzi ya moyo huwa hayana mpinzani. 

Mambo mengi yanayotokea katika maisha ya mwanadamu, moyo ndio chimbuko la kila jambo. Mara zote usipouzuia moyo, unaweza ukajikuta unafanya maamuzi ya kujilaumu.

Moyo unaongea na kukuelekeza nini ufanye. Unaweza kumugundua mtu kama kuna jambo analifikiria pale utakapo angalia kwenye paji lake la uso. Mtu huyo anaweza kuwa anawaza mambo chanya au hasi. 

Endapo utamshitua mtu huyo na ukaona anashtuka na kuguna, basi elewa kabisa kuwa hapo alikuwa mbali sana na ulimwengu huu. Mara nyingi hilo analofikiria linakuwa halina majibu. Na kama kutakuwa na majibu, basi majibu hayo yatakuwa hasi. Moyo unaua na kuhuisha. Moyo ndio kila kitu, moyo ndio uhai wenyewe.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Cha Mtu Mavi

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Tunaishi duniani kwa viwango tofauti vya maisha. Kuna baadhi ya watu wanavyo vitu vya kupitiliza, hadi inakuwa kama kufuru. Wengine wanavyo vya wastani, na wengine wanavyo kidogo au hawana kabisa. Kutokana na hali hiyo wanadamu tunaishi kwa kutoridhika na hivyo tulivyo navyo.

Kutokana na hizi hali mbalimbali, binadamu wengine huanza kujawa na hisia za wivu au chuki kwenye mioyo yao na hata kuwapelekea kutoa maamuzi magumu na mabaya kwa jirani, rafiki na hata kwa ndugu zao. Maamuzi magumu na mabaya yanaweza kumshawishi mtu kujiuliza, “kwa nini yeye na siyo mimi”? Hali hiyo inamshawishi mtu kuingiwa na roho ya uharibifu mpaka inampelekea kuiba mali za wengine au kufanya nambo mengine mabaya, ili mradi mwenye chake aumie.

Lakini na mhusika pia, ambaye ndiye mtenda maovu, pia huishia kupata kesi na kuishia kufungwa. Hata familia yake hudhalilika sana kutokana na uovu wake. Hali kadhalika, tunashuhudia mifarakano mingi kutoka kwa marafiki. jamaa na hata kwenye koo zetu. Amani na upendo baina ya binadamu hutoweka kutokana tu na wivu wa mtu anapoona mwenziye ana hiki na kile na yeye hana chochote. Dunia ni ya ajabu, imejaa wivu, husuda na mambo mengi mabaya yanayotendwa na binadamu.   

Usemi huo wa ‘Cha mtu mavi’, unatufundisha kuwa turidhike na tulicho nacho. Endapo na wewe unataka kuwa navyo vingi kama vya yule, basi yakupasa ufanye kazi kwa bidii ili upate mafanikio. Kufanya uharibifu siyo njia sahihi ya wewe kufanikiwa. Vilevile yakupasa ujue kwamba cha fulani siyo chako. Endapo utakitamani, ni bora ukione kinanuka kama mavi. Kwa kufanya hivyo, ile hali ya kufanya maovu halafu upate kesi au uishie jela itakuepuka na hivyo utakuwa na maisha ya amani ndani ya moyo wako na mambo mengine yataendelea vizuri. Utaishi bila misukosuko kutokana na kutamani vya watu na kufanya uovu.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Thamani Ya Mbwa Huisha Mwisho Wa Mawindo

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Ni ukweli usiopingika kuwa katika maisha thamani ya mtu huisha pale anapokuwa hayuko tayari tena ama hana uwezo wa kuendelea kutoa msaada. Hii inaweza kutokea kutokana na hali yake kiuchumi kupungua au kutetereka.

Katika kipindi hicho hata kama ulikuwa mtoaji kila mtu uliyemsaidia anaweza kuwa mbali na wewe, ataanza kujitenga. Kama ni mtu asiye na imani, mathalani, kuwa na Mungu, mtu anayepitia mikasa kama hiyo, hii anaweza kuchanganyikiwa na kufa mapema kwa usongo wa mawazo na magonjwa mengine sambamba na hayo. 

Dunia hii ni ya ajabu, pia ni kitu dhaifu sana, lakini usicheze nacho. Dunia inaweza ikakudanganya na hata kukutoa kwenye msitari. Wakati huo hata thamani yako inaweza isiwepo tena.

Sambamba na usemi huu kuna ule unaosema, “Mkono mtupu haulambwi”. Kwa mwindaji, mbwa huwa ni wa muhimu sana anapoenda kuwinda. Mara amalizapo na kupata mawindo yake, mbwa anakuwa hana thamani tena kwake. Inaweza ikatokea pia, endapo mbwa huyo atamsogelea binadamu huyo, anaweza hata akampiga na kumfukuza ili akakae mbali naye. 

Hii ni tabia ni ya ajabu kwa binadamu. Wakati wanaelekea kuwinda mbwa huyo alikuwa wa muhimu sana kwake. Alikuwa akimbembeleza na kumfanya kama rafiki yake wa kweli.

Binadamu ndivyo tulivyo kwenye hii dunia, mara nyingi tunampenda mtu wakati tuna uhitaji naye. Tatizo likiisha huwa hatumkumbuki yule aliyetufikisha hapo na mara nyingi huwa hatuna haja nae tena. 

Pamoja na uzuri wake, dunia hii ni chombo dhaifu sana, chombo chenye vurugu nyingi na za kutosha. Tusipokuwa waangalifu, tunaweza tukajikuta mahali pabaya. Yatupasa kuchukua tahadhari ili tuweze kuendana nayo.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Tuache Ukatili Kwa Wanyama, Malipo Ni Hapa Hapa Duniani

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Palikuwa na kijana mmoja ambaye alirithi mifugo kutoka kwa baba yake. Hivyo alikuwa mfugaji na mchungaji. Miongoni mwa mifugo aliyorithi, walikuwepo punda, ng’ombe, mbuzi, kondoo, mbwa na kadhalika. Akiwa machungani alikuwa na tabia mbaya ya kuitesa baadhi ya mifugo yake. Moja kati ya wanyama aliyekuwa anateswa sana ni punda ambaye alikuwa anamsadia kubeba mizigo.

Siku moja alimziba punda mdomo, akamfunga kamba shingoni kisha akamfungia kwenye mti. Alianza kumpiga kwa kutumia fimbo, makofi na mateke. Mateso na maumivu hayo yalipozidi na kuwa makali sana, punda alipandisha hasira. Alimgeuzia kibao mwanadamu huyo katili. Naye alianza kumrushia mateke ya nguvu. Hatimaye alimng’ata kwenye mguu, akawa anazunguka naye hadi mguu ukavunjika.

Kijana alipata maumivu makali sana. Alijuta kutenda ukatili huo kwa mifugo yake. Aliahidi kutorudia tena matendo hayo maovu.

Simulizi hii inaendana na methali zifuatazo; “Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu uchungu”, “Mtenda, hutendwa”, na “Mwosha, huoshwa.”

Hapo tunajifunza kutokuwa wakatili kwa mifugo yetu. Mifugo nayo ina miili ambayo huumia pale inapofanyiwa ukatili.

Isitoshe, yatupasa tutambue kuwa wanyama wana haki zao za msingi zinazowalinda. Haki hizo ni pamoja na kulishwa, kutunzwa vizuri, kupatiwa maji ya kutosha na kutibiwa pindi wakiugua. Hali kadhalika, wanahitaji kuwekwa kwenye mabanda mazuri na safi ya kulala. Kwa ujumla, wanahitaji mazingira safi. 

Hali kadhalika, ikumbukwe kuwa mifugo tunayofuga ni kwa matumizi na faida yetu sisi binadamu. Hivyo, inatulazimu kuacha ukatili kwa mifugo yetu.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

%d bloggers like this: