Mama Sixtha Komba (M&E Officer, TEWWY) atuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na uwanja wa majadiliano hasa kati ya vizazi.
Author Archives: Wisdom&Wellness
BUSARA ZIANGUKIAZO KWENYE “T” TATU
Mama Sixtha Komba anatueleza juu ya T tatu ambazo unaweza tumia katika kuyakabili matatizo ukutananayo. Akianza na fafanuzi juu ya T tatu. T1 ni Tatizo T2 ni Tatuzi T3 ni Tokeo Mama Sixtha Komba anaendelea kufafanua hizi T tatu katika nyanja mbili, hasi na chanya kwa kutumia mfano wa mwanafunzi aliyefeli mitihani yake na jinsiContinue reading “BUSARA ZIANGUKIAZO KWENYE “T” TATU”
MOYO WA MTU NI KICHAKA
Magreth KayomboWisdom&Wellness Counselor Kibo, Dar-es-Salaam Moyo huficha siri nyingi, nzuri na mbaya. Ni vigumu kwa mtu kuelewa undani wa mtu mwingine.
USIIGE KUNYA KWA TEMBO UTAPASUKA MSAMBA
Magreth KayomboWisdom&Wellness Counselor Kibo, Dar-es-Salaam Msemo huu ni onyo kwa wanaopenda kuiga bila kufikiri.
UZURI WA MKAKASI NDANI NI KIPANDE CHA MTI
Magreth KayomboWisdom&Wellness Counselor Kibo, Dar-es-Salaam Usiwe mwepesi kudanganywa na unachokiona nje, ndani kinaweza kisiwe kizuri. Ni vema kuchukua muda na kukichunguza kwa kina ili kujiridhisha.
KUVUJA KWA PAKACHA NAFUU KWA MCHUKUZI
Magreth KayomboWisdom&Wellness Counselor Kibo, Dar-es-Salaam Kususia jambo linalohusu jamii au hata mtu mwingine kwa sababu ya tatizo binafsi kunaleta unafuu kwa wale wanaobakia. Kwa upande mwingine inaweza kuwa ni maneno ya kujifariji wewe mwenyewe baada ya watu kukususa.
MTU MWENYE AIBU HUFIA UPENUNI MWA NYUMBA
Paulina NgwawasyaWisdom&Wellness Supervisor Ilala & Kinondoni, Dar-es-Salaam Ni vema kushirikisha watu matatizo yanayokusibu ili upate msaada na usifikie pabaya.
USITUKANE WAKUNGA NA UZAZI UNGALIPO
Margareth KayomboWisdom&Wellness Counselor Kibo, Dar-es-Salaam Hutumika kama onyo kwa mtu anae dharau huduma muhimu anayopewa, kwani siku nyingine ataihitaji tena. Usemi huu unaweza kufananishwa na ule usemao “Baniani mbaya kiatu chake dawa.”
NJIA NDEFU HUTUPA MAISHA MAREFU
Caroline SwaiWisdom&Wellness Supervisor Kigamboni,Kinondoni & Ubungo, Dar-es-Salaam Tunapotaka kufanya jambo lolote tuwe na subira, tusiharakishe kwani haraka haina baraka. Tunapovuta subira tunapata muda wa kutafakari na kufanya kwa umakini na hatima yake ni mafanikio mazuri.
WAKATI UKUTA
Caroline SwaiWisdom&Wellness Supervisor Kigamboni,Kinondoni & Ubungo,Dar-es-Salaam Inatufundisha kuwa kila jambo linatakiwa kufanyika kwa wakati wake kama lilivyopangwa. Vinginevyo ukichelewa, utakosa mengi, unaweza pata hasara na itakuwa haina maana kwako. Msemo huu unafanana na ule usemao “Chelewa chelewa utakuta mwana si wako”.