Tuko katika ulimwengu wenye vurugu na fujo zisizohesabika. Kila mtu anacho akijuacho ambacho anaona mwingine hakijui na wala hakiwezi. Ni fikira ambazo wanadamu tunatembea nazo. Furaha na huzuni ni sehemu ya maisha yetu.
Monthly Archives: April 2023
Mtu Hufurahia Shida Zako, Sio Furaha Yako
Matatizo yameumbwa na kila mtu huyapata. Hakuna mtu ambaye hajawahi kupitia matatizo, na hayuko ambaye hatayapitia. Inategemea ni tatizo gani na wakati gani linakutokea.
Ishi Kadri Unavyojaliwa, Na Sio Kama Mwingine Anavyoishi
Watu wengi wana kawaida ya kupenda kujilinganisha na watu wengine. Watu kama hao hupenda kujiuliza, “kama yule yuko hivi, kwa nini na mimi nisiwe vile?”
Tujifunze Kusamehe
Alikuwepo mama mmoja ambaye alikuwa mwalimu wa shule ya msingi. Mama huyu alibahatika kupata mtoto wa Kike ambaye aliweza kumsomesha hadi Chuo Kikuu. Baada ya kuhitimu shahada yake, alimtafutia kazi nzuri.
Njia Ya Mkato Tamu, Lakini Ina Madhara
Mara nyingi kama mtu anataka afike haraka, anatafuta njia ya kukatisha, njia ya haraka. Njia hiyo inaweza kuwa nzuri pale tu utakapofanikiwa kufika kule uendako. Kuna wakati lakini njia ya mkato inaweza ikakupoteza na ukashindwa kufika uendako. Kuna baadhi ya binadamu, hupenda kutafuta mafanikio kwa kupitia njia ya udanganyifu, kama kutapeli wenzao.
Tuwe Wastaarabu Na Busara Katika Maongezi
Binadamu tunatakiwa kuishi kwa kufuata taratibu fulani zilizopo kwenye jamii, hii ni pamoja na jinsi tunavyozungumza na wenzetu. Kwa maana hiyo, ukiwa mstaarabu na mwenye busara huwezi kuuliza uliza watu maswali ambayo hayastahili kuulizwa, maswali kama: ‘Bado hujaolewa tu?….Una watoto wangapi?…Utazaa lini?…Mbona umri umeenda?…na mengine mengi.
Usimkumbushe Mtu Mema Yako, Acha Dunia Imkumbushe
Kusaidiana katika maisha yetu ni jambo la kawaida. Hapa duniani tunategemeana. Hakuna aliyekamilika.
Hekima Ni Jambo La Msingi
Kile unachokiita baraka au ushindi kilianza kama tatizo. Mara nyingi, yule anayefanikiwa kutatua matatizo huonekana kama ana baraka au mshindi fulani hivi. Ni kawaida kwa kila mwanadamu kupata matatizo. Pale mtu anapopata matatizo, ni vema kutafuta mbinu za kupambana nayo. Wengi hujaribu kukimbia matatizo yanapotokea.
Ukishindwa Hili Leo, Kesho Utashinda Lile
Wakati sisi tunasoma shule ya msingi, ilikuwa ni madarasa manne tu, yaani la kwanza hadi la nne. Enzi hizo walizingatia sana umuhimu wa kila darasa kuwa na wanafunzi wasiozidi arobaini na tano.
Huwezi Kupanda Ngazi Ya Mafanikio Ukiwa Umeweka Mikono Mfukoni
Ni jukumu la binadamu wote kuwajibika katika maisha yetu ya kila siku. Huwezi ukafanikiwa bila kutoka jasho. Kufanya kazi kwa bidii, ndio siri kubwa ya mafanikio ya mwanadamu.