Caroline SwaiWisdom&Wellness Supervisor Kigamboni,Kinondoni & Ubungo, Dar-es-Salaam Tunapotaka kufanya jambo lolote tuwe na subira, tusiharakishe kwani haraka haina baraka. Tunapovuta subira tunapata muda wa kutafakari na kufanya kwa umakini na hatima yake ni mafanikio mazuri.
Monthly Archives: January 2021
WAKATI UKUTA
Caroline SwaiWisdom&Wellness Supervisor Kigamboni,Kinondoni & Ubungo,Dar-es-Salaam Inatufundisha kuwa kila jambo linatakiwa kufanyika kwa wakati wake kama lilivyopangwa. Vinginevyo ukichelewa, utakosa mengi, unaweza pata hasara na itakuwa haina maana kwako. Msemo huu unafanana na ule usemao “Chelewa chelewa utakuta mwana si wako”.
MKWE/KIJANA ALIYEOA KWENU UTAMJUA KWA MAVAZI YAKE
Grace MshangaWisdom&Wellness Supervisor Temeke & Ubungo, Dar-es-Salaam Mvulana aliyeoa katika familia yenu lazima awe nadhifu, aongee kwa heshima, awe na juhudi katika kazi – hivi ndivyo vitu vitakavyomtambulisha kuwa ni mkwe wenu anayefaa.
JITAHIDI KUWA NA MARAFIKI WAZURI WENGI LAKINI AMINI WACHACHE WANAOKUFAA
Christina MandeWisdom&Wellness Counselor Kizinga, Dar-es-Salaam Marafiki wazuri watakuunga mkono kwa mambo yote mema unayofanya au unayofikiri kufanya na pia kutokushabikia kufanya maovu. Hawatasita kukuambia ukweli pale utakapofanya au kufikiria kufanya maovu na daima watakuelekeza njia inayofaa.
UMOJA NI NGUVU, UTENGANO NI UDHAIFU
Caroline SwaiWisdom&Wellness supervisor Kigamboni,Kinondoni & Ubungo, Dar-es-Salaam Tunaposhirikiana kufanya shughuli zetu pamoja, inakuwa rahisi kumaliza haraka kuliko ya kipekee na kujitenga – hali ambayo inachukua muda mrefu na kupunguza ufanisi.
CHAKULA KIIVAPO WATOTO HUWA WANAKIZUNGUKA HARAKA, LAKINI WAKATI WA KAZI HUTOA SABABU NYINGI
Watoto wajifunze kazi ndogondogo za nyumbani tangu umrÄ™ mdogo.
MMOJA SHIKA SI KUMI NENDA UJE
Sakina BushiriWisdom&Wellness Counselor Mangaya, Dar-es-Salaam Usiache au kudharau kitu ambacho tayari unacho mkononi ukitegemea utapata vingi baadaye.
ULIMI NI PAMBO LA MDOMO
Mary KinguWisdom&Wellness Meditation Garden Tandale, Dar-es-Salaam Ulimi ni kiungo muhimu katika mazungumzo ya kila siku, unapotumiwa vibaya huleta madhara makubwa. Usemi huu unatupa fundisho la kutumia vizuri ulimi katika mazungumzo, iwe kwenye familia, jamii, na hata katika taasisi mbalimbali.
MFA MAJI HAACHI KU TAPATAPA
Christina MandeWisdom&Wellness Counselor Kizinga, Dar-es-Salaam Msemo huu huwaasa wale wote ambao wakianguka katika mipango yao usingizia mambo mengi kama watu wanamwonea wivu, wanamloga, hawampendi n.k. Hapo anaangalia alipoangukia bila kuchunguza sababu zizotuangusha ili tuzitatue na kuanza upya.
LAITI NINGELIJUA KABLA
Caroline SwaiWisdom&Wellness Supervisor Kigamboni, Kinondoni & Ubungo,Dar-es-Salaam Hii inawaasa wale wanaopenda kufanya mambo kwa pupa bila kufikiria kwa kina na mara nyingi huishia pabaya wakiwa na majuto.