Utaula Wa Chuya Kwa Uvivu Wa Kuchagua

Grace Mshanga - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Grace Mshanga (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Chuya ni mpunga ambao unakuwa umejichanganya na mchele mzuri ambao upo tayari kwa kupikwa. Hizo chuya huwa zinatakiwa kuchaguliwa ili kupata mchele mzuri, tayari kwa kupikwa. Lakini inawezekana kwa watu wengine ambao ni wavivu, kuupika mchele ukiwa hivyo haujachaguliwa wasione tofauti ama vibaya.

Usemi huu unatufundisha kutokuwa wavivu katika jambo lolote tunalolifanya. Kila mtu anatakiwa kufanya kazi kwa kujituma ili kufanikisha malengo yake. Unapofanya jambo kwa ulegevu unaukaribisha umaskini wa kukutosha. 

Hata mabinti zetu wana tabia ya kuchagua wenzi wao wa aina fulani mwisho wanaishia kupata watu ambao sio saizi yao. Mara nyingi huwa wanaishia kuula wa chuya. Tunashauriwa kuwa makini wakati wote tunapotakiwa kufanya uchaguzi. Dunia ni kitu dhaifu sana, hata hivyo, hatutakiwi kuichezea.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Nyani Akiumwa Ukimpa Dawa Akipona, Jiandae Mahindi Yako Kuliwa

Avelina Hokororo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Avelina Hokororo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Nyani ni mnyama anayekaa porini. Anafanana na ngedere au kima. Anakula sana mahindi yakiwa shambani. 

Kuna ndugu anaweza kuja kwako akiwa hoi kimaisha, hata hela ya kula hana. Safari yake ni kuja kuomba msaada. Unampokea na kukaa naye nyumbani kwako. Anakula kile ambacho Mungu amekujalia hapo nyumbani pako. 

Baada ya siku kadhaa unampa mtaji wa pesa. Anaanzisha biashara yake ukiwa naye hapo nyumbani pako. Hatimaye anafanikiwa. Anahama pale nyumbani pako na kwenda kujitegemea sehemu nyingine. 

Kutokana biashara ile uliyomuanzishia, maisha yake yanakuwa ya juu kuliko hata ya kwako. Sasa badala ya kukushukuru, anaanza kukudharau na kukutangazia ubaya kwa watu kuwa ulikuwa unamnyanyasa sana. Anakuona kuwa hufai kwa lolote, na kwamba wewe si chochote mbele yake.

Simulizi hii inafundisha kuwa siyo wote utakaowasaidia watakuja kukumbuka kwa mema yako. Mfano wa nyani mgonjwa kwenye simulizi hii, ni yule mtu aliyekuja kuomba msaada kwako. Kwa huruma unampa dawa (pesa) akapona. Sasa baadaye anakuja kukushambulia kwa dharau za kupitiliza. 

Hii ni sawa na usemi usemao: “Tenda wema uende zako,  usingoje shukurani”. Kuna binadamu wengi ambao wana tabia kama hii ya utovu wa shukurani. Yatupasa tuwavumilie tu na kutowajali kwani wako wengi hao. 

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection 

Furaha Ni Kama Marashi Kwani Huongeza Maisha

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Wahenga wa kale walisema, “Kitu furaha ni sawasawa na marashi”, kwani huwezi kujipulizia wengine wasisikie harufu yake. Hii inajidhihirisha wazi kwamba ukiwa na furaha huwezi kuificha kwani mtu yeyote atakayekuona atatambua kuwa umefurahi au una furaha. Basi, endapo wewe umefurahi, jitahidi na watu wengine nao wafurahi kutokana na furaha yako.

Hata siku moja usikubali kufurahi au kuruhusu kupata raha baada ya kuona shida, maumivu, machungu au maanguko ya mtu mwingine. Yaani usifurahie kuteseka kwa mwenzio, kwa mfano, kufiwa, kupata ajali, kuuguliwa, kupata mikosi, uchumi kuporomoka, kuibiwa au kufeli shule.

Hapa tunapata funzo kuwa, ukiwa na furaha siku zote mshirikishe au mwambukize mwenzio, ndugu yako, rafiki au jirani kwani furaha huongeza au hurefusha maisha ya binadamu, kinyume chake ni makasiriko au hasira ambazo husababisha msongo wa mawazo, na kusononeka ambapo hatima yake ni maamuzi hasi kama vile, kujinyonga, kujirusha dirishani au kujidhuru kwa njia moja au nyingine. 

Hivyo, sisi kama binadamu, furaha ni kitu muhimu sana inatakiwa iwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku kwa ajili ya kutuongezea siku zetu za kuishi hapa duniani.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Usitegemee Uzuri Wako Maana Kuna Siku Utazeeka

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Wako mabinti zetu wengi ambao wanajiona ni wazuri kwa umbo na sura. Watu hao mara nyingi hujiona kuwa ni bora zaidi kuliko wengine. Na huwa wanapenda hata kuchagua ni nani watakuwa wenzi wao. 

Wengi hupenda kutafuta watu wenye uwezo na ambao wamefanikiwa katika maisha. Lakini huwa hawajali au hawapendi kujua kuwa hao wanaowapapatikia wamefikaje pale walipo. Tamaa hiyo inawafanya kuwa na wapenzi wengi. Hapo kunakuwa na mashindano, kila mtu anavutia kwake ili aonekane mzuri zaidi ya mwingine. 

Tabia hii ya kuruka ruka huwafanya mabinti wengi wasahau kuwa kuna kuzeeka. Kadri wanavyozidi kujichelewesha na umri nao unazidi kuyoyoma. 

Kikubwa kinachotakiwa ni kujiheshmu na kuwa na tabia nzuri. Kwa kufanya hivyo ndipo unaweza kuimarika. Hali kadhalika, Muumba wako naye hatimaye, atakupatia yule aliyekuandalia kuwa mwenza wako, yule ambaye atakuwa wako milele.

Kuna mifano hai mingi ya mabinti kujidanganya. Tunaona kwenye mtandao kinachoendelea kuhusu kijana aliyejirusha kutoka ghorofani. Eti kuna mabinti zaidi ya wawili, kila mmoja anajiona kuwa ana haki zaidi ya kutambuliwa kuwa ndiye aliyekuwa mwenza wa huyo kijana. Lakini kwa bahati mbaya, katika hao mabinti wawili, hakuna ambaye alijaliwa kuzaa na yule kaka. Inasemekana mmoja kati yao ameishi na huyo kijana kwa miaka minne, na mwingine miaka mitatu. Kuna mwingine aliishialipiwa hata mahari, lakini hakuna aliyezaa nae. Hali hii imeleta vurugu tosha. 

Haieleweki kwa nini yule kaka aliamua kuishi maisha ya namna hiyo. Kila binti aliyehojiwa anaongea lake, anavutia upande wake. Yaonekana kijana huyu alikuwa ni kama tegemeo la kila mmoja wao. Kifo chake kimekuwa ni pigo kubwa kwao. Nguzo imeanguka kwa wote. 

Kila mmoja amebaki kujilaumu na kujiuliza, “kwa nini alijichelewesha kusonga mbele?”Kijana alikuwa mtanashati, mtoaji, lakini siyo muoaji. Mabinti waliponzeka na utanashati wake, waliehuka na utoaji wake. Leo wanalia, wamebaki na majuto.

Tunakumbushwa kuwa tusipende vya kuvikuta, bali ni vema ukaanza naye toka kwenye sifuri, mkajenga pamoja taratibu, lakini mwisho wa siku mtakavyochuma vitakuwa vyetu nyote wawili. Mabinti wanaaswa kuondoa kiburi cha uzuri. Tabia nzuri ndio iwe ngao ya maisha ya mtu yeyote.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Anayekukosoa, Anakujenga!

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Ni kawaida ya watu wengi kupenda kuonekana kuwa wako mbele sana katika kila jambo wanalolifanya. Hakuna mtu anayetaka kuonekana kuwa hawezi.

Ni ubinadamu kabisa kwa mwanadamu kupenda kusifiwa kuliko kurekebishwa. Inawezekana kabisa kuwa mtu anafanya mambo ambayo hayawapendezi watu, lakini anakuwa hayuko tayari kurekebishwa. Endapo atatokea mtu wa kumkosoa, basi ataanza visa kuhusu huyo mtu na hata anaweza kuanza kumsema vibaya. Mara nyingi, hapo ndipo chuki huanzia. 

Katika maisha yetu, inatupasa kukubali na kuwa tayari kukosolewa. Kukosolewa kunamtengeneza mtu.  Unapokubali kukosolewa unakuwa na uhakika wa maisha ya baadae. Tukumbuke kuwa maisha ni kama ngazi kubwa, usipopanda vizuri, utateleza na kuanguka. Na ukianguka utabaki kujilaumu, oh fulani aliniambia, nk. Mwisho inabaki ni majuto tu.

Kubali kuonywa. Usimkasirikie anayekuonya maana anakuelekeza namna ya kuenenda na mwisho utafanikiwa katika hilo jambo. Hakuna aliyefanikiwa bila ya kupitia misukosuko. 

Tupende kuelekezwa, tusichukie tunapoonywa maana hata maandiko matakatifu yanatusihi kusikiliza maonyo na kuyatendea kazi kwani ndipo ushindi wetu ulipo.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Mpe Adui Yako Tabasamu Badala Ya Machozi

Victoria Nakajumo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Victoria Nakajumo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Unaporuhusu uchungu na maumivu ndani yako ni rahisi sana kuchoka na kukataa tamaa. Usibebe kila kitu, na wala usichukulie kila kitu kwa uzito, utaelemewa. 

Kuna mambo unahitaji kuyapuuzia. Usitake kujua kila unachofanyiwa na adui zako na watesi wako. Mengine acha yapite kama vile hujayasikia na kama vile, hayakuhusu.

Unapomuonesha adui yako machozi yako na uchungu, unasababisha adui ajisifie, ajione yeye ni bora na kwamba ‘amekuweza’.

Lakini unapompuuza adui yako, unamfanya akose nguvu na hatimaye atachoka kukufuatilia. Kwa hiyo usiubebeshe moyo wako na nafsi yako mizigo isiyo ya lazima. Kwa kubeba kila ambacho adui yako anakufanyia, utajichosha.

Jipe utaratibu wa kupuuzia baadhi ya mambo ili moyo na nafsi yako viwe huru. Binadamu ni kiumbe wa ajabu, usimuendekeze, utajiumiza bure.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection 

Kubali Kupoteza Ili Uende Viwango Vingine

Victoria Nakajumo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Victoria Nakajumo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Katika maisha unaweza kupoteza nafasi, au watu uliowaamini sana. Pengine hata uliweza kufikiri kuwa bila wao maisha au malengo yako hayatafanikiwa.

Sio kila unayempoteza au kila unachopoteza ni hasara kwako. Ni kweli kabisa ukiambiwa neno hili katikati ya maumivu hauwezi kuelewa, ila baada ya muda utagundua lina ukweli ndani yake.

Kuna vitu vingine, lazima upoteze kwanza ili upate vingine. Hali kadhalika, kuna mabadiliko ambayo ni lazima yatokee kwanza ili uwe vile unavyotaka kuwa.

Kuna watu ni lazima waondoke kwenye maisha yako au wawe mbali zaidi ili usogee hatua ya mafanikio.
Usiwang’ang’anie watu ambao unatakiwa kuachana nao. Usilazimishe kuwepo mahali ambapo unatakiwa kuondoka. Usililie vitu ambavyo unatakiwa kuviacha. Kila kitu huja kwa kusudi maalumu, lazima tulijue hilo. Maisha ndivyo yalivyo.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection 

Maisha Ni Kutegemeana

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Maisha ya mtu ni fumbo zito. Kila mtu ana umuhimu katika maisha ya mwenzake. Hii ni kwa sababu maisha ni kutegemeana. 

Unayemwona hakufai kwa hili leo, anaweza akakufaa kwa lile wakati mwingine. Hata mtu awe maskini kiasi gani, bado anaweza kuwa na umuhimu kwa mtu mwingine, kama siyo kwako. Kuna wakati ambapo anaweza kutoa msaada kwa mwenzake, ukabaki unashangaa.

Pia hata kama wewe ni tajiri wa kujitosheleza usijigambe kamwe kwa kuwaambia watu wewe huhitaji msaada kutoka kwa mtu yeyote. Kwani hiyo siyo kweli kabisa.

Hivyo usimdharau binadamu mwenzio. Kama ni kutoa msaada, wewe toa tu bila masharti, kinyongo au kubagua.

Hata ukiwa na madaraka, kipato kizuri na nafasi ya juu ofisini au mahali popote, hurakiwi kumdharau mtu. Unayemuona hafai leo, kesho unaweza ukamhitaji na anaweza kukusaidia pia. Kwa hiyo, tunapaswa kujenga ushirikiano na wenzetu katika mazingira yoyote yawayo.

Hapa tunapata funzo kuwa, hakuna binadamu aliye kamilika. Hivyo hakuna mtu anayeweza kuishi peke yake. Binadamu sote tunategemeana kwa namna moja ama nyingine. Tumeumbwa ili tusaidiane na hivyo kutegemeana ndio utaratibu wa maisha yetu sisi wanadamu. Hata hivyo isitoshe, safari yetu yetu ni fupi sana. Yatupasa tuutumie muda wetu wa hapa duniani vizuri, kwa kadiri ya uwezo wetu.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Wakati Mwingine Hawakupendi, Wanakupenda Kwa Kile Ulicho Nacho

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Ni ukweli usiopingika kuwa watu humpenda mtu mwenye nacho. Watu wa aina hii, yaani wale wenye nacho, huwa na marafiki wengi kupita maelezo. Ukweli huu huonekana zaidi kama huyo mtu atakuwa ni mtoaji sana na ambaye anapenda kusaidia watu. 

Mara nyingi watu hupenda kuwafuatilia watu wenye hali hiyo, yaani wale wenye nacho. Watu hawa hujitahidi kuonyesha upendo wa ajabu na pia huwamwagia sifa nyingi watu ambao wanacho.  

Maisha ya mwanadamu ni yale ya kupanda na kushuka, hilo halikwepeki. Pale ikitokea kuwa mambo yameenda vibaya, basi wale watu wote waliokuwa wakimfuatilia kwa mbwebwe na vifijo,  

hutokomea kabisa. Kuanzia hapo, hakuna mtu atakayemsogelea tena. Sababu kubwa ya kukimbiwa ni kutokana na ukweli kwamba hana kitu tena na hana msaada kwao tena. Watu hao watatokomea mmoja baada ya mwingine. na watakuwa hawana mpango na wewe tena. 

Endapo hapo nyuma ulikuwa umeomba msaada kutoka kwao, sasa itabaki kuwa ni kejeli tu na masimango. Huu ndio ulimwengu ulivyo, ulimwengu tunamoishi sisi wanadamu. 

Kwa kawaida, sisi binadamu hatuna shukurani hata kidogo. Ukitenda wema usitegemee kurudishiwa fadhila. Pamoja na yote, wewe tenda mema tu huku ukijua kuwa  shukurani hazitakuwepo. Hali kadhalika, tuwe na kiasi katika kusaidia watu maana

 binadamu ni wa ajabu, wana matatizo na shida nyingi. Siyo rahisi kuwajua, kwani hubadilika kila uchao.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Heri Shetani Unayemjua, Kuliko Malaika Usiyemjua

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor – TEWWY).

Tupo duniani tukizungukwa na watu mbalimbali na wenye tabia tofauti tofauti. Tunaishi kwa kutegemeana maana sisi ni wanadamu ndiyo maana utaona watu wanasaidina kwa shida na raha. Zaidi ya hapo utaona kwenye jamii zetu, kuna watu wanaishi kwa kupendana kama ndugu na kufanya vitu pamoja na kushauriana kwa kila jambo linalokuja mbele zao.

Naamini tumeshuhudia hilo Mmakonde anakuwa na urafiki na Mchaga na wakaishi kwa upendo na kwa kushibana sana.

Unakuja wakati hali hiyo inabadilika. Utakuta majaribu yanajipenyeza na kuanza kuharibu umoja wao na kuanza kugombana na kutengana, na urafiki unavujika kwa lugha chafu na wakaanza kuonana kama maadui.

Ikifikia hali hiyo kila mtu anaenda upande wake na kuanza kutafuta rafiki mwingine ambae wataendana. Zaidi ya hapo tumeshuhudia wengi wakifikia maamuzi hayo, urafiki haudumu kwasababu uliyokuwa unayategemea yanakuwa sivyo. Mwisho unaanza kujilaumu na kusema, afadhali ningebaki na rafiki yangu wa awali.

Mara nyingi yanatukuta hayo kwa kukosa ufahamu wa kutambua kuwa wote ni binadamu na hakuna aliyekamilika. Jambo jepesi ni kuombana msamaha yaishe na mahusiano yaendelee. Mwisho inapelekea kumkumbuka uliyemwona shetani kuliko huyo uliyemuona malaika kwako.   

Kutokana na msemo huo nina ushauri kuwa dunia imejaa mapito, lakini msamaha na kuachilia, utaishi kwa amani ndani ya jamii. Mahusiano na watu wengine yatakuwa mazuri na uhakika wa kufanya mambo mbalimbali ya maendeleo, hayatakuwa magumu kwako.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

%d bloggers like this: