Mama Sixtha Komba (M&E Officer, TEWWY) atuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na uwanja wa majadiliano hasa kati ya vizazi.
Wazazi na walezi wanahitaji kuweka mahusiano mazuri yanayo ruhusu majadiliano kati ya mzazi na mtoto ili kuhamasisha maamuzi yenye mwafaka, kwa mfano: uchaguzi wa shule, kozi, mchepuo wa masomo, kazi, mke na kadhalika. Kuwa na mazungumzo ya wazi yamsaidia mtoto azingatie hilo swala maana naye alikua sehemu ya mjadala pia. Hii usaidia kupunguza migogoro katika familia na jamii kwa ujumla na uhimiza utendaji wa moyo msafi.
Mama Sixtha Komba anatueleza juu ya T tatu ambazo unaweza tumia katika kuyakabili matatizo ukutananayo. Akianza na fafanuzi juu ya T tatu.
T1 ni Tatizo
T2 ni Tatuzi
T3 ni Tokeo
Mama Sixtha Komba anaendelea kufafanua hizi T tatu katika nyanja mbili, hasi na chanya kwa kutumia mfano wa mwanafunzi aliyefeli mitihani yake na jinsi wazazi wanavyolipokea swala hilo.
Matumizi hasi ya T tatu
T1 ambayo ni Tatizo – Kijana kafeli mtihani
T2 ambayo ni Tatuzi – Wazazi/walezi wanamkasirikia na kuamua kumfukuza nyumbani
T3 ambayo ni Tokeo – Kijana anaingia mtaani na kujiingiza kwenye makundi mabaya kama uvutaji bangi, wizi, unywaji wa pombe kupita kiasi au kuamua kujidhuru.
Matumizi chanya ya T tatu
T1 ambayo ni Tatizo – Kijana kafeli mtihani
T2 ambayo ni Tatuzi – Wazazi/walezi wanaamua kumtia moyo kijana wao na kutaka kujua kwanini alifanya vibaya ili wamsaidie.
T3 ambayo ni Tokeo – Kijana baada ya kutiwa moyo na wazazi/walezi anaamua kurudi shule akiamini atafanya vizuri na atakuwa msaada katika jamii, kwani mti mmoja hauanguki mara mbili.
Contact Us
Don’t hesitate to reach out with the contact information below, or send a message using the form.
Kususia jambo linalohusu jamii au hata mtu mwingine kwa sababu ya tatizo binafsi kunaleta unafuu kwa wale wanaobakia. Kwa upande mwingine inaweza kuwa ni maneno ya kujifariji wewe mwenyewe baada ya watu kukususa.
Hutumika kama onyo kwa mtu anae dharau huduma muhimu anayopewa, kwani siku nyingine ataihitaji tena. Usemi huu unaweza kufananishwa na ule usemao “Baniani mbaya kiatu chake dawa.”
Tunapotaka kufanya jambo lolote tuwe na subira, tusiharakishe kwani haraka haina baraka. Tunapovuta subira tunapata muda wa kutafakari na kufanya kwa umakini na hatima yake ni mafanikio mazuri.
Inatufundisha kuwa kila jambo linatakiwa kufanyika kwa wakati wake kama lilivyopangwa. Vinginevyo ukichelewa, utakosa mengi, unaweza pata hasara na itakuwa haina maana kwako. Msemo huu unafanana na ule usemao “Chelewa chelewa utakuta mwana si wako”.